SOMO: UTUMISHI KATIKA UFALME WA MUNGU

lengo:

1: kuelewa Msingi wa wito wa utumishi wa Kiroho

2: kuelewa sifa na tabia zinazopaswa kuonekana kwa mtumishi wa kiroho Kristo akiwa kielelezo na kigezo.

3: kuelewa changamoto, thawabu na hatima ya utumishi wa kiroho


🔹MADA: MSINGI NA WITO WA UTUMISHI

Lengo la Siku ya Kwanza

  • Kuelewa maana halisi ya utumishi wa Kikristo
  • Kutambua kuwa kila Mkristo ameokoka ili atumike
  • Kuweka msingi wa kibiblia wa utumishi

1. Maana ya Utumishi wa Kikristo

Utumishi wa Kikristo ni:

  • Kujitoa kwa Mungu kwa moyo wote. Warumi 12:1
  • Kutimiza mapenzi ya Mungu kwa kuwahudumia watu. Zaburi 40:8; Yohana 4:34, 5:30, 6:38
  • Kuishi kwa ajili ya Kristo, si kwa ajili ya nafsi. 2 Wakorintho 5:15; Wagalatia 2:20

Fundisho kuu: Utumishi ni mwitikio wa wokovu, si njia ya kuupata wokovu.

2. Chanzo cha Utumishi: Wito wa Mungu

Hakuna mtu anayetumika bila kuitwa.

Waebrania 5:4 – Hakuna mtu ajitwaliaye heshima hii
Yeremia 1:5 – Kabla hujazaliwa nalikujua
Yohana 15:16 – Sinyi mlionichagua, bali mimi niliwachagua

Yapo Mambo ya msingi katika Utumishi

👉 Utumishi:

  • Una wito (calling)
  • Una kusudi (purpose)
  • Una mpango (assignment)

1. WITO (CALLING)

Maana ya Wito

Wito ni mwito wa Mungu kwa mtu kuingia katika maisha ya kumtumikia Yeye.
Ni uamuzi wa Mungu, si wa mwanadamu. Wito hutangulia huduma, vipawa, au ofisi.

“Si ninyi mlionichagua, bali mimi niliwachagua ninyi…” (Yohana 15:16)

Asili ya Wito

  • Wito unatoka kwa Mungu (Waebrania 5:4)
  • Ni wa neema, si matendo (Warumi 11:29)
  • Huambatana na uwajibikaji mkubwa (Yakobo 3:1)

Aina za Wito

  1. Wito wa wokovu – kila mtu (2 Petro 3:9)
  2. Wito wa jumla wa utumishi – waamini wote (1 Petro 2:9)
  3. Wito maalum – huduma fulani (Yeremia 1:5; Wagalatia 1:15)

Sifa za Wito

  • Hauondolewi kirahisi. Angalia kwa Yona anajaribu kukimbia lakini BWANA anamfuatilia. Soma Yona yote
  • Huleta mzigo wa rohoni. “Utawezaje kutulia, ikiwa BWANA amekupa agizo?” (Yeremia 47:7)
  • Huonekana hata kabla ya mtu kujitambua (Paulo – Matendo 9)

📌 Bila wito → huduma huwa kazi ya kibinadamu, si ya kiroho.

2. KUSUDI (PURPOSE)

Maana ya Kusudi

Kusudi ni sababu kuu kwa nini Mungu anakuita. Ni “kwa ajili ya nini?” ya utumishi wako.

“Kwa maana sisi tu kazi yake, tuliumbwa katika Kristo Yesu tupate kutenda matendo mema…” (Waefeso 2:10)

Kusudi Hutofautiana na Wito

  • Wito ni mwito wa kuwa mtumishi
  • Kusudi ni sababu ya utumishi huo

Mifano ya Kusudi

  • Musa – kuwaokoa Israeli (Kutoka 3:10)
  • Yeremia – kuwa nabii wa mataifa (Yeremia 1:5)
  • Paulo – kupeleka Injili kwa Mataifa (Matendo 9:15)

Kusudi Huleta:

  1. Mwelekeo – kutambua cha kufanya
  2. Motisha – nguvu ya kuendelea
  3. Mipaka – hukusaidia kusema hapana kwa mambo yasiyo yako

“Nitakimbia kuelekea shabaha…” (Wafilipi 3:14)

📌 Bila kusudi → utumishi huwa wa kuhangaika bila matokeo ya kudumu.

3. MPANGO (ASSIGNMENT)

Maana ya Mpango

Mpango ni kazi au jukumu maalum Mungu analokupa kwa wakati, mahali, na watu fulani.
Mpango unaweza kubadilika, lakini wito hubaki.

“Kuna wakati wa kila jambo…” (Mhubiri 3:1)

Mpango Hutegemea:

  • Mahali (location)
  • Wakati (season)
  • Kiwango cha ukuaji wa mtumishi

Mifano ya Mpango

  • Daudi:
    • Kwanza mchungaji wa kondoo
    • Baadaye shujaa
    • Hatimaye mfalme
  • Paulo:
    • Antiokia
    • Safari za kimisionari
    • Hatimaye gerezani akiandika nyaraka

Sifa za Mpango

  • Hubadilika kulingana na msimu.
  • Huhitaji utiifu wa sasa. “Nalifanya haraka wala sikukawia, kuyatii maagizo yako” (Zaburi 119:60)
  • Huthibitishwa na matunda (Matendo 13:2–3)

📌 Tatizo kubwa: watu wengi wanapenda mpango bila kuelewa wito na kusudi.

MUHTASARI WA TOFAUTI

KipengeleMaelezoHubadilika?
WitoMwito wa Mungu kuwa mtumishi❌ Hapana
KusudiSababu ya kuitwa❌ Mara chache
MpangoKazi/eneo maalum kwa wakati✅ Ndiyo

HITIMISHO

✔ Wito → NANI umeitwa kuwa
✔ Kusudi → KWA NINI umeitwa
✔ Mpango → NINI unafanya sasa

“Mtu aitwaye na Bwana, na aendelee katika wito wake.” (1 Wakorintho 7:20)

3. Kila Muumini Ameitwa Kutumika

Hakuna Mkristo “mtazamaji” katika ufalme wa Mungu.

1 Petro 2:9 – Ukuhani wa kifalme
1 Petro 4:10 – Kila mmoja na karama yake
Waefeso 4:7 – Neema imepewa kila mmoja

Hitimisho la siku ya kwanza:
👉 Kama umeokoka, umeitwa kutumika.


🔹 SIKU YA PILI: Ijumaa 16/01/2026

MADA: MFANO WA YESU NA TABIA ZA MTUMISHI WA KWELI

Lengo la Siku ya Pili

  • Kumtazama Yesu kama kigezo cha utumishi
  • Kujifunza tabia za lazima za mtumishi
  • Kufahamu gharama ya utumishi

1. Yesu Kristo – Mtumishi Mkamilifu

Yesu ni Bwana, lakini alichagua kuwa mtumishi.

Marko 10:45 – Hakuja kuhudumiwa bali kuhudumia
Wafilipi 2:5–8 – Alitwaa mfano wa mtumwa
Isaya 53:11 – Mtumishi wangu mwenye haki

Ebrania 12:1-3  Tumtazame Yesu aliyestahimili mapingamizi

Mfano wa vitendo: Yohana 13:3–15 – Yesu ananawisha miguu ya wanafunzi

👉 Hakuna kazi ndogo katika utumishi wa kweli.

2. Tabia za Mtumishi wa Kweli

(a) Unyenyekevu. Mathayo 23:11–12; Yakobo 4:10

(b) Uaminifu. 1 Wakorintho 4:1- 2; Mathayo 25:21

(c) Utii. 1 Samweli 15:22; Yohana 14:15

(d) Upendo.  1 Wakorintho 13:1–3; Yohana 13:34–35

3. Gharama ya Utumishi

Utumishi wa kweli una gharama. Hivyo ni muhimu kujua ili tusijeshindwa Luka 14:25-33

  1. Kujikana nafsi: Luka 9:23. Hapa ni kule kukubali kufa yaani kuufisha utu wa kale Kol 2:20, 3:1-5
  2. Kupata mateso kwa ajili ya Kristo: 2 Timotheo 3:12, Mdo 16:23, 2 Kor 11:23, kol 1:24-25; 2 Wakorintho 6:4–10 – Paulo aeleza mateso ya utumishi

👉 Usipotaka gharama, hujawa tayari kwa utumishi.


🔹 SIKU YA TATU: Shule ya Jumapili 19/01/2026

MADA: CHANGAMOTO, TUZO NA HATIMA YA UTUMISHI

Lengo la Siku ya Tatu

  • Kuelewa changamoto za utumishi
  • Kujua jinsi ya kudumu katika utumishi
  • Kutambua thawabu za milele za utumishi

1. Changamoto Katika Utumishi

Kama mtumishi wa Mungu utakutana na changamoto zenye lengo la kuyateteresha maadili yako na Imani yako. Zifuatazo ni baadhi ya changamoto hizo

  1. Upinzani na Chuki: – Hata unapofanya mema, unaweza kukutana na watu wasiokuelewa na wakakupinga. “Nanyi mtachukiwa na watu wote kwa ajili ya jina langu; lakini mwenye kuvumilia hata mwisho, ndiye atakayeokoka” (Mathayo 10:22)
  2. Kishawishi cha kiburi: Unapofanikiwa kuna hatari ya kujitwalia utukufu badala ya kumrudishia Mungu. “Kijapo kiburi ndipo ijapo aibu; Bali hekima hukaa na wanyenyekevu” (Mithali 11:2),
  3. Uchovu wa mwili na roho (Burnout): – Kuna hali ya kuchoka kimwili kutokana na mambo mengi ambayo yanaweza kukukabili katika utumishi.Marko 6:31, Isaya 40:29 – 31
  4. Kukata tamaa: – Mtumishi anweza kuchoka na kukata tamaa anapoona matunda hayaji upesi. “Tena tusichoke katika kutenda mema; maana tutavuna kwa wakati wake, tusipozimia roho” (Gal 6:9), Luka 18:1
  5. Mashambulizi ya adui: – Mtumishi daima yupo katika vita na shetani katika ulimwengu wa roho hivyo anawindwa daima na shetani akimzungukia daima hivyo kuwa makini sana mtengemee Mungu daima. 1 Petro 5:8-9

Namna ya Kudumu Katika Utumishi

  1. Kaa ndani ya Yesu Kristo:- Yohana 15:4–5
  2. Mtegemee Kristo daima: Waebrania 12:1–3
  3. Tumia kwa halali neno la Kweli (Kristo): – 2 Timotheo 2:15

Msingi wa kudumu:

  • Maombi
  • Neno
  • Ushirika
  • Unyenyekevu

2. Tuzo/thawabu za Utumishi

 (Biblia inafundisha kuwa utumishi haupotei bure) Kol 3:24-25, Marko 10:29 – 30  

“Maana Mungu si dhalimu hata aisahau kazi yenu na pendo lile mlilolidhihirisha kwa jina lake…” – Waebrania 6:10

MISINGI YA KIBIBLIA YA TUZO

(a) Mungu ni Mlipaji wa Huduma: Utumishi wote wa kweli una malipo kutoka kwa Mungu, si lazima kwa wanadamu.

“Basi thawabu yako itakuwa kubwa.” (Luka 6:35)

“Baba yako aonae sirini atakulipa.” (Mathayo 6:4)

📌 Utumishi usiotambuliwa na watu bado unatambuliwa na Mungu.

(b) Tuzo si wokovu: Ni muhimu kufahamu:

  • Wokovu ni kwa neema (Waefeso 2:8–9)
  • Tuzo ni kwa uaminifu katika utumishi (1 Wakorintho 3:8) “Kila mtu atapokea thawabu yake mwenyewe, kwa kadiri ya kazi yake.”

AINA ZA TUZO ZA UTUMISHI

Tuzo/thawabu za kiroho zinaanza hapa duniani kupitia baraka, lakini kilele chake  ni mbinguni.

A. TUZO ZA SASA (DUNIANI)

Hizi hutolewa na Mungu wakati mtu bado yuko duniani.

1. Furaha na Amani ya Ndani: Mtumishi wa kweli hupokea furaha isiyohusiana na mazingira.

“Furaha ya Bwana ndiyo nguvu yenu.” (Nehemia 8:10)

“Amani ya Mungu ipitayo akili zote…” (Wafilipi 4:7)

📌 Utumishi huleta mateso, lakini pia huleta furaha ya kipekee.

2. Uthibitisho wa Mungu (Divine Approval): Mungu humshuhudia mtumishi wake kwa:

  • matunda
  • ushuhuda wa Roho
  • kuthibitisha kazi yake

“Huyu ni Mwanangu mpendwa, ninayependezwa naye.” (Mathayo 3:17)

3. Ukuaji wa Kiroho na Mamlaka: Kadiri mtu anavyotumikia kwa uaminifu:

  • hukua kiroho
  • hupewa mamlaka zaidi: utumishi wa unyenyekevu huleta kibali na kuinuliwa (Mathayo 23:11)

“Aliye mwaminifu katika yaliyo madogo…” (Luka 16:10)

4. Baraka za Mahitaji (sio anasa): Mungu hutunza watumishi wake. Mungu anaahidi kuwabariki wale wanaotumika kwa uaminifu (Kutoka 23:25)“Utafuteni kwanza ufalme wa Mungu… na hayo yote mtazidishiwa.” (Mathayo 6:33).

B. TUZO ZA MBINGUNI (ZA MILELE) – Taji

Hizi ndizo tuzo kuu za utumishi. “Jiwekeni hazina mbinguni…” (Mathayo 6:20).

Tutapokea taji katika Kiti Cha Hukumu cha Kristo (Bema Seat).  Hapa si hukumu ya wokovu, bali ya tuzo za kazi.

“Kwa maana imetupasa sisi sote kudhihirishwa mbele ya kiti cha hukumu cha Kristo, ili kila mtu apokee ijara ya mambo aliyotenda kwa mwili, kadiri alivyotenda, kwamba ni mema au mabaya.” — 2 Wakorintho 5:10

“…Moto utaijaribu Kazi ya kila mtu, kazi yako ikikaa utapata thawabu, ikiteketea unapata hasara( utakosa tuzo), bali utaokolewa kama kwa moto (Yaani huna kitu).” (1 Wakorintho 3:13 – 15)

📌 Kazi:

  • ya dhahabu → italipwa
  • ya majani → itateketea

 AINA YA TAJI (CROWNS) ZA KIBIBLIA

Biblia inataja aina tano ya taji kama tuzo za uaminifu.

1. Taji Isiyoharibika. Kwa wale walio na nidhamu na kujikana 1 Wakorintho 9:25

Hutolewa kwa watumishi wanaodhibiti miili yao na tamaa za dunia kwa ajili ya huduma.

2. Taji ya Furaha (Soul Winner’s Crown). Kwa wale wanaoleta watu kwa Kristo

“Maana tumaini letu, au furaha yetu, au taji ya kujionea fahari, ni nini? Je! Si ninyi, mbele za Bwana wetu Yesu, wakati wa kuja kwake?” (1 Wathesalonike 2:19).  Ni tuzo ya wahubiri, wamisionari, na mashahidi wa Injili.”Na walio na hekima watang’aa kama mwangaza wa anga; na hao waongozao wengi kutenda haki watang’aa kama nyota milele na milele” (Dan 12:3)

3. Taji ya Haki. Kwa wale wanaopenda kurudi kwa Kristo 2 Timotheo 4:8

Hutolewa kwa wanaoishi maisha ya utakatifu wakingojea Bwana.

4. Taji ya Uzima. Kwa kuvumilia majaribu na mateso Yakobo 1:12; Ufunuo 2:10

Hasa kwa walioteswa kwa sababu ya imani. Kumbuka “Mateso ya mwenye haki ni mengi, lakini BWANA humponya nayo yote” (Zaburi 34:21)

5. Taji ya Utukufu isiyokauka. Kwa wachungaji, viongozi na watumishi waaminifu. 1 Petro 5:2–4

Kwa wanaochunga kondoo si kwa faida bali kwa moyo wa kuitwa.

 VIGEZO VYA KUPEWA TUZO

Mungu hatoi tuzo kwa:
❌ umaarufu
❌ ukubwa wa huduma
❌ sifa za watu

Bali kwa:
✔ uaminifu (Mathayo 25:21)
✔ nia ya moyo (1 Wakorintho 4:5, Wakolosai 3:23-24)
✔ utiifu (1 Samweli 15:22)

 HATARI YA KUPOTEZA TUZO

Mtu anaweza: kuokoka, lakini akakosa tuzo

“Akiokolewa, lakini kama kwa moto.” (1 Wakorintho 3:15)

“Shikeni sana msije mkapoteza thawabu yenu.” (2 Yohana 1:8)

NOTE:-

✔ Utumishi una gharama
✔ Lakini una tuzo ya sasa na ya milele
✔ Hakuna kazi ya Bwana isiyolipwa

“Basi, ndugu zangu wapendwa, mwimarike, msitikisike, mkazidi sana kutenda kazi ya Bwana siku zote kwa maana mwajua ya kwamba taabu yenu siyo bure katika Bwana.” — 1 Wakorintho 15:58

  • Hatima ya Utumishi wa Kiroho

Hatima ya mtumishi wa koroho ni hesabu atakayotoa mbele ya Muumba wake kuhusu karama na nafasi alizopewa.

  1. Kuhukumiwa kwa uaminifu:- Hatima haitegemei ukubwa wa cheo, bali uaminifu katika kile kidogo ulichopewa. “Bwana akamwammbia, vema, mtumishi mwema na mwaminifu; ulikuwa mwaminifu kwa machache, nitakuweka juu ya mengi; ingia katika furaha ya Bwana wako”(Mathayo 25:21, 2 Wakorintho 5:10)
  2. Kurithishwa Ufalme:- Hatima ya mwisho ya Mtumishi wa Kweli ni kupumzika baada ya kazi ngumu ya duniani. 2 Timotheo 4:7 – 8

Hitimisho la jumla

Utumishi:

  • Ni safari, si tukio
  • Ni utiifu, si umaarufu, kwa sasa wako watu wengi wanatafuta umaarufu na Viewers kwenye mitandao
  • Ni kwa ajili ya Kristo, si wanadamu

Wakolosai 3:23–24; Yoshua 24:15. Ili mtumishi ashinde changamoto na afikie hatima njema, maandiko yanatupa siri moja kubwa: Nia ya Moyo. “Lo lote mfanyalo, lifanyeni kwa moyo, kama kwa Bwana, wala si kwa wanadamu, mkijua ya kuwa mtapokea kwa Bwana ujira wa urithi. Mnamtumikia Bwana Yesu Kristo”(Wakolosai 3: 23 – 24)

🔔 WITO WA MWISHO

👉 Mungu anatafuta watumishi waaminifu, si watu mashuhuri.

SOMO: KUJIANDAA KWA KURUDI KWA YESU KRISTO (UNYAKUO)

Lengo la Somo: Kujenga ufahamu wa kina juu ya uhakika wa ahadi ya kurudi kwa Kristo na kumpa muumini zana za kiroho za kuishi maisha ya utakatifu wakati akingojea unyakuo.


1. Uhakika wa Ahadi ya Kurudi Kwake

Mtume Petro alijua kuwa kadiri muda unavyopita, watu wataanza kutilia shaka kurudi kwa Yesu.

  • Kushinda Kebehi (2 Petro 3:3-4): Petro anaonya kuwa siku za mwisho watakuja wenye kudhihaki wakisema, “Iko wapi ahadi ya kuja kwake?” * Mtazamo wa Mungu wa Muda (2 Petro 3:8): Kwa Bwana siku moja ni kama miaka elfu. Kuchelewa kwake si ulegevu, bali ni uvumilivu ili watu wengi wapate kutubu (2 Petro 3:9).
  • Uhakika wa Neno: Kama vile dunia ya kwanza ilivyoangamizwa kwa maji, neno lile lile limeuweka ulimwengu wa sasa kwa ajili ya moto siku ya hukumu (2 Petro 3:7).

2. Jinsi Unyakuo Utakavyotokea

Ili kuliandaa kanisa, ni lazima kuelewa asili ya tukio hili:

  • Ghafla (1 Wathesalonike 5:2): Siku ya Bwana inakuja kama mwizi usiku. Hakutakuwa na tangazo la mapema kwenye vyombo vya habari.
  • Mabadiliko ya Miili (1 Wakorintho 15:51-52): Kwa dakika moja, kufumba na kufumbua, tutabadilishwa. Miili hii ya uharibifu itavaa kutoingia uharibifu.
  • Sauti ya Malaika (1 Wathesalonike 4:16-17): Bwana mwenyewe atashuka, na wale waliokufa katika Kristo watafufuka kwanza, kisha sisi tulio hai tutanyakuliwa pamoja nao mawinguni.

3. Maandalizi: Tuishi Vipi Tukiwa Tunangojea?

Petro anauliza swali la msingi katika 2 Petro 3:11: “Imewapasa ninyi kuwa watu wa tabia gani katika mwenendo mtakatifu na utauwa?”

A. Maisha ya Utakatifu na Bila Mawaa

  • 2 Petro 3:14: “Fanyeni bidii ili mwonekane mbele zake katika amani, bila mawaa wala doa.” Hii inamaanisha kukataa dhambi za siri na kuishi maisha yanayompendeza Mungu.
  • 1 Petro 1:15-16: Kuwa watakatifu kwa sababu Yeye aliyetuita ni mtakatifu.

B. Kukesha na Kuomba

  • 1 Petro 4:7: “Mwisho wa mambo yote umekaribia; basi, iweni na akili kamilifu, mkeshe katika kuomba.” Maombi hutunza moto wa kiroho usizime.

C. Upendo wa Ndugu

  • 1 Petro 4:8: Zaidi ya yote, pendaneni kwa juhudi, kwa kuwa upendo husitiri wingi wa dhambi. Kanisa linalongojea unyakuo ni kanisa lenye umoja na upendo.

4. Tuzo ya Wale Wanaongojea

Mtume Petro anatuhakikishia kuwa subira yetu si ya bure:

  • Taji ya Utukufu (1 Petro 5:4): “Na Mchungaji Mkuu atakapodhihirishwa, mtaipokea taji ya utukufu, ile isiyonyauka.”
  • Mbingu Mpya na Nchi Mpya (2 Petro 3:13): Tunatazamia makao ambapo haki yakaa ndani yake.

HITIMISHO NA WITO

Unyakuo si tukio la kuogofya kwa mwaminifu, bali ni siku ya ukombozi. Maandalizi hayafanyiki siku ya tukio, bali ni maisha ya kila siku ya toba na utii.

Dokezo la Kutafakari: Je, ikiwa parapanda italia dakika tano zijazo, hali yako ya kiroho ikoje?

📖 Nguvu ya Neno la Mungu na Uzoefu wa Mateso


📖 Nguvu ya Neno la Mungu na Uzoefu wa Mateso


Utangulizi: Mtazamo wa Petro

Petro, mwandishi wa Nyaraka za Kwanza na Pili, alikuwa akiongea na waumini waliozoea mateso na kunyanyaswa kwa ajili ya imani yao. Katika hali hiyo ngumu, jambo moja lililoendelea kuwatia moyo na kuwatuliza ni Neno la Mungu. Somo hili linaangazia jinsi Neno la Mungu linavyotoa nguvu, matumaini, na mwelekeo hata tunapopitia majaribu.


I. Nguvu ya Neno la Mungu Katika Kuzaliwa Upya

Petro anaanza kwa kuweka msingi wa maisha ya Kikristo, ambao ni kuzaliwa upya, na anafafanua chanzo cha uzima huo:

  • Petro 1:1:23: “Maana mmekwisha kuzaliwa mara ya pili; si kutokana na mbegu iharibikayo, bali isiyoharibika, kwa Neno la Mungu lililo hai, lidumulo hata milele.”
    • Uchambuzi: Neno la Mungu si kitu cha muda mfupi, bali ni mbegu isiyoharibika ambayo inaleta uzima wa milele (uzima mpya).
    • Nguvu ya Neno: Linatufanya tuwe viumbe vipya, tukitoka katika utumwa wa dhambi na kuingia katika uhuru na utakatifu.
  • Kupanua (Yakobo 1:18): “Kwa kupenda kwake alituzaa sisi kwa Neno la kweli, ili tuwe kama matunda ya kwanza ya viumbe vyake.” Hii inaonesha kuwa Neno ndilo chombo cha Mungu cha kutuleta katika uhusiano naye.

II. Neno Kama Msingi Thabiti Katika Mateso

Wakati mateso yanapotokea, Neno la Mungu linabaki kuwa kiini cha tumaini na utulivu wetu.

  • Petro 1:1:6-7: “Mnafanya furaha sana, ijapokuwa sasa kwa kitambo kidogo, ikiwa ni lazima, mmehuzunishwa kwa majaribu mengi; ili kwamba kujaribiwa kwa imani yenu…”
    • Mtazamo wa Petro: Anafahamu kuwa mateso (majaribu) yatakuja.
  • Petro 1:1:24-25: “…kwa maana Wote wenye mwili ni kama majani, na utukufu wake wote ni kama ua la majani. Majani hunyauka, na ua huanguka; bali Neno la Bwana hudumu milele.”
    • Nguvu ya Neno: Dunia, mwili, na mateso ni ya muda mfupi (kama majani), lakini Neno la Mungu linadumu milele. Nguvu yetu katika mateso haitoki kwa hali ya kibinadamu (inayoharibika), bali katika Neno la Mungu (lisiloharibika).
  • Kupanua (Mathayo 7:24-25): “Basi, kila mtu asikiaye maneno yangu haya, na kuyafanya, mfano wake ni mtu mwenye akili, aliyejenga nyumba yake juu ya mwamba… mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, pepo zikavuma, zikaipiga nyumba ile, wala haikuanguka; kwa maana ilikuwa imejengwa juu ya mwamba.”
    • Neno ni Mwamba: Neno la Mungu ni msingi thabiti (Mwamba) unaotuwezesha kusimama hata wakati wa “dhoruba” za mateso.

III. Neno la Kinabii Linaloweka Imani Wazi

Katika Nyaraka ya Pili, Petro anahimiza waumini kushikilia Neno kwa sababu linatoa uhakika kamili wa ukweli wa Kristo, kinyume na mafundisho ya uongo yaliyokuwa yakianza kuibuka.

  • Petro 2:1:19-21: “Nasi tuna lile Neno la unabii lililo imara zaidi; nanyi mwafanya vema kulizingatia; kama taa ing’aayo mahali penye giza, hata kutakapopambazuka, na nyota ya asubuhi kuzuka mioyoni mwenu…”
    • Uhakika Kamili: Petro anasema Neno la Mungu (unabii) ni imara zaidi kuliko hata uzoefu wa kibinafsi (mfano: kumwona Kristo katika Mlima wa Kugeuka Sura).
    • Taa Katika Giza: Katika giza la mateso, mashaka, na mafundisho ya uongo, Neno linafanya kazi kama taa inayoonesha njia. Linatoa mwelekeo wakati hatuelewi nini kinatokea.
  • Petro 2:3:15-16: Anazungumzia jinsi maandiko mengine (ya Paulo) yanavyokuwa magumu, lakini bado ni Neno la Mungu ambalo linahitaji kutafutwa na kufafanuliwa kwa uangalifu.
    • Uzoefu wa Mateso na Mafundisho ya Uongo: Mojawapo ya mateso makubwa ni kupoteza mwelekeo. Neno linatuweka imara dhidi ya wale wanaopotosha ukweli kwa manufaa yao.

IV. Mwito wa Kuitikia Neno Katika Mateso

Petro anahitimisha kwa wito wa vitendo, akisisitiza jinsi tunavyopaswa kuitikia Neno la Mungu tunapopitia mateso.

  1. Tamani Neno:
    • Petro 1:2:2: “Kama vitoto vichanga, tamani sana maziwa ya akili yasiyoghoshiwa, ili kwa hayo mpate kukua mpaka wokovu.”
    • Kitendo Katika Mateso: Katika mateso, mara nyingi tunatamani faraja za ulimwengu. Badala yake, tunahimizwa kutamani Neno ili kuimarisha na kukomaza imani yetu.
  2. Kuwa Mtakatifu (Maisha yanayoendana na Neno):
    • Petro 1:1:15-16: “Bali kama yeye aliyewaita alivyo mtakatifu, nanyi mnatakiwa kuwa watakatifu katika mwenendo wenu wote; kwa sababu imeandikwa, Mtakuwa watakatifu, maana mimi ni mtakatifu.”
    • Mateso na Utakatifu: Mateso yanajaribu imani, lakini Neno linatuita tuendelee kuishi maisha matakatifu. Nguvu ya Neno inatuwezesha kutembea katika utakatifu hata katika hali ya adha.
  3. Kumbuka Neno (Kutoka Petro 2:3:1-2):
    • “Ninyi wapenzi, sasa nawaandikia waraka huu wa pili; katika yote miwili nawahimiza akili zenu safi kwa kuwakumbusha; mkumbuke maneno yaliyotangulia kusemwa na manabii watakatifu, na ile amri ya Bwana Mwokozi iliyoletwa na mitume wenu.”
    • Kitendo Katika Mateso: Mateso huweza kufanya tusahau ahadi za Mungu. Petro anatukumbusha kuwa kukumbuka Neno ndio kinga dhidi ya kulegea.

Hitimisho

Neno la Mungu ni zaidi ya historia; ni uzima, mwamba, na taa yetu. Tunapopitia uzoefu wa mateso (iwe ni ugonjwa, matatizo ya kifamilia, au kunyanyaswa kwa ajili ya imani), tunapaswa kurudi kwenye Neno ambalo linadumu milele. Nguvu yetu si katika kuepuka shida, bali katika uwezo wa Neno la Mungu wa kutuimarisha katikati ya shida.

MAADILI NA NIDHAMU YA KIROHO KWA MKRISTO

Somo: Maadili na Nidhamu ya Kiroho kwa Mkristo

Kichwa kidogo: Kuishi Maisha Safi Katika Kristo

Maandiko ya Kifungu Kikuu: 1 Wakorintho 6:18-20; 1 Wakorintho 10:31; 1 Wakorintho 9:24-27

Ujumbe wa Somo:
Mkristo anatakiwa kuishi maisha ya maadili mema na nidhamu ya kiroho kwa sababu mwili wake ni hekalu la Roho Mtakatifu, na kila tendo lake linaathiri ushuhuda wake na utukufu wa Mungu.


Hoja Kuu 1: Mwili wa Mkristo ni Hekalu la Roho Mtakatifu

Andiko: 1 Wakorintho 6:19-20 – “Je! Hamjui kwamba miili yenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, mliopewa na Mungu, na kwamba hamjawiwa wenyewe? Kwa maana mmelipwa kwa gharama; kwa hiyo mtii Mungu katika miili yenu.”

Maelezo:

  • Mwili wa Mkristo si mali ya kawaida; ni hekalu la Mungu.
  • Hii inamaanisha kuwa kila tendo la kimwili au kiroho linapaswa kuonyesha heshima na hofu ya Mungu.
  • Dhambi za kimwili au tamaa zisizo na nidhamu zinaharibu hekalu hili na kushusha heshima ya imani.

Mfano:

  • Kila kitendo tunachokifanya, kama kutumia maneno, kushirikiana na wengine, au hata kula na kunywa, kinaweza kuwa kitendo cha heshima kwa Mungu au kidhambi. Mfano moyo kulemewa na ulafi, ulevi na masubufu ya dunia Luka 21:34, 35, War 13:13

Hoja Kuu 2: Epuka Dhambi na Ndoto/tamaa za Mwili

Andiko: 1 Wakorintho 6:18 – “Epuka uzinzi. Kila dhambi ya mtu yeyote inatoka nje ya mwili; lakini yule anaye kufanya uzinzi anakiuka mwili wake.”

Maelezo:

  • Uzinzi ni mfano wa tamaa za mwili zisizo na nidhamu.
  • Dhambi ya kimwili ina madhara ya kiroho na mara nyingi inaathiri maisha yote ya Mkristo, ikiwa ni pamoja na ushuhuda wake mbele ya wengine. Mfano Mfalme Daudi kitendo cha kuzini na Mke wa Uria kilisababisha matatizo mengi mno kwake, familia yake na Taifa kwa ujumla 2 Sam 12:1-14
  • Nidhamu ya kiroho inamaanisha kudhibiti tamaa na kuishi kwa heshima ya Mungu, kwa kuzingatia mipaka ya Biblia tikiwezeshwa na neema ya Mungu. War 13:11-14, Tit 2:11-13

Hoja Kuu 3: Kila Kitendo Kifanyike Kwa Utukufu wa Mungu

Andiko: 1 Wakorintho 10:31 – “Kwa hiyo, mkile, mkinywa, au mkifanya kitu kingine, fanyeni yote kwa utukufu wa Mungu.”

Maelezo:

  • Nidhamu ya kiroho inajumuisha kufanya kila jambo kwa heshima na utukufu wa Mungu, si kwa maslahi yetu binafsi au kujipendekeza kwa watu. Miili yetu itumike kwa utukufu wa Bwana
  • Hii inahusisha mambo madogo na makubwa: maneno, matendo, kazi, hata starehe.
  • Mkristo aliye na nidhamu ya kiroho anafanya kila jambo kwa nia ya kumtukuza Mungu. 1 Kor 6:12-17, Wakolosai 1:10, 3:23, 24

Hoja Kuu 4: Nidhamu ya Kiroho inahitaji Ushirikiano wa Akili na Mwili

Andiko: 1 Wakorintho 9:24-27 – “Hamjui kwamba katika mbio zote wanabashiri wote wanakimbia, lakini mmoja anapata tuzo? Kimbieni ili mupate. Kila mtu anayekimbia anadhibiti mwili wake; ili si kama atakuwa akimwaga kwa bure. Nimiye kama asiye na nidhamu, mimi nawafunga mwili wangu na kuwafanya wanyenyeke, nisipokuwa mimi mwenyewe nikipotea.”

Maelezo:

  • Paulo anafananisha maisha ya kiroho na mbio za riadha. Mkristo anapaswa kudhibiti tamaa, mazoea mabaya, na tabia zisizo za kiroho.
  • Nidhamu ya kiroho inahitaji mazoezi makali, kusali, kujizuia, na kuzingatia mafundisho ya Biblia. 1Tim 4:7,8; Ebra 12:11
  • Hii inatupa ushindi wa kiroho na kuimarisha ushuhuda wa Kikristo.

Hoja Kuu 5: Matokeo ya Maadili na Nidhamu

Maandiko: 1 Wakorintho 10:12-13 – “Kwa hiyo, mtu yeyote akidhani kuwa amesimama, aangalie asipate kuanguka. Hakika hakuna majaribu yaliyokukuta isipokuwa yale ya kawaida kwa wanadamu; lakini Mungu ni mwaminifu, hatakuruhusu mtihani ukuzidi uwezo wenu, bali atatupatia njia ya kutoka ili tuweze kustahimili.”

Maelezo:

  • Nidhamu ya kiroho hutoa mkingo wa kuepuka dhambi na kuishi maisha ya ushuhuda.
  • Mungu hutoa nguvu na njia ya kustahimili kila jaribu.
  • Mkristo aliye na nidhamu ya kiroho ana amani ya moyo na heshima kwa Mungu na watu. War 5: 1

Hitimisho

  • Maadili na nidhamu ya kiroho ni msingi wa maisha ya Kikristo.
  • Mwili wetu ni hekalu la Roho, matendo yetu lazima yawe kwa utukufu wa Mungu.
  • Nidhamu inahitaji mazoezi ya kiroho, kujizuia, na kushirikiana na Mungu kila siku.
  • Kwa kuishi maisha yenye maadili na nidhamu ya kiroho, Mkristo anaweza kushuhudia imani yake kwa nguvu, na kufurahia tumaini la milele.

Imeandaliwa na Mwalimu Anselemi Mashimba Alloyce

WhatsApp +255747 251 929

NGUVU YA MUNGU KATIKA UDHAIFU WETU

SOMO: NGUVU YA KRISTO KATIKA UDHAIFU WETU

Andiko Kuu: 2 Wakorintho 12:1–10. “Neema yangu yakutosha; kwa maana nguvu yangu hukamilika katika udhaifu.” (2 Wakorintho 12:9)

UTANGULIZI

Wapendwa katika Kristo Yesu, maisha ya Mkristo siyo safari ya raha na mafanikio ya kila siku, bali ni njia yenye majaribu, udhaifu, na maumivu, ambamo Mungu anajifunua kwa namna ya ajabu.
Mtume Paulo anatufundisha kwamba udhaifu si kushindwa, bali ni mwangalizo wa nafasi ya nguvu ya Mungu kufanya kazi ndani yetu.

MAANA YA UDHAIFU KIBIBLIA.

Udhaifu ni Kukosa Uwezo wa Kujitegemea Bila Mungu

Biblia inafundisha kwamba udhaifu wa kweli ni kutambua kwamba bila Mungu hatuwezi chochote.

📖 Yohana 15:5 “Mimi ni mzabibu, ninyi matawi; akaaye ndani yangu, nami ndani yake, huyo huzaa sana; kwa maana pasipo mimi ninyi hamuwezi kufanya neno lo lote.”

Hivyo udhaifu sio tu hali ya kushindwa, bali ni kutambua uhalisia wetu wa kibinadamu — kwamba nguvu, hekima, na uhai wote hutoka kwa Mungu. Na kutambua udhaifu huleta unyenyekevu ndani yetu kwa Mungu wetu

Kwa Kigiriki neno linalotumika katika 2 Wakorintho 12:9 ni “astheneia” likimaanisha: kutokuwa na nguvu, kutokuwa na uwezo, au hali ya udhaifu wa kimwili, kiroho, au kihisia.

1. MUNGU HUFUNUA SIRI KWA WANYENYEKEVU

📖 2 Wakorintho 12:1–4. Paulo alipata ufunuo wa mbinguni ya tatu, lakini hakujivuna — alikaa mnyenyekevu. Mungu alijua moyo wake na alihakikisha Paulo anabaki katika unyenyekevu kwa kumpa “mwiba katika mwili.”

Maandiko ya Kusaidia:

  • Yakobo 4:6: “Mungu huwapinga wenye kiburi, bali huwapa neema wanyenyekevu.”
  • Mithali 11:2: “Kujivuna huleta aibu, bali hekima iko kwa wanyenyekevu.”

Funzo:
Watu wengi wanapobarikiwa na ufunuo, au karama, huanza kujisifu kana kwamba ni kwa uwezo wao. Mungu, kwa hekima yake, huwaruhusu kupitia mambo yanayowakumbusha kuwa bado ni wanadamu. Hivyo, unyenyekevu ni kinga dhidi ya kuanguka kiroho.

2. MWIBA KATIKA MWILI NI SEHEMU YA SAFARI YA IMANI

📖 2 Wakorintho 12:7–8. Paulo alipewa “mwiba” ili asijiinuwe kupita kiasi. Haijulikani hasa ulikuwa ni ugonjwa, mateso, au mapambano ya kiroho — lakini ilikuwa ni hali iliyomtesa sana.

Maandiko ya Kusaidia:

  • Ayubu 23:10: “Lakini ajua njia nitembeayo; akishanijaribu, nitatoka kama dhahabu.”
  • Zaburi 119:71: “Imenifaa kuteseka, ili nipate kujifunza maagizo yako.”
  • Warumi 8:28: “Na tunajua ya kuwa katika mambo yote Mungu hufanya kazi pamoja na wale wampendao kwa mema.”

Funzo:
Kuna mateso ambayo Mungu huruhusu si kwa adhabu, bali kwa mafunzo ya kiroho.
Mwiba unatusaidia tusisahau tunamtegemea Mungu, si sisi wenyewe.
Kama vile dhahabu inavyosafishwa kwa moto, vivyo hivyo imani yetu inakua kupitia majaribu.

3. MAOMBI YASIYOJIBIWA KWA NJIA TUNAYOTARAJIA: Maombi yakizanayo na kusudi la Mungu

📖 2 Wakorintho 12:8. Paulo aliomba mara tatu Bwana auondoe ule mwiba, lakini Mungu hakufanya hivyo. Badala yake alimjibu: “Neema yangu yakutosha.”

Maandiko ya Kusaidia:

  • Yesu mwenyewe aliomba: “Baba, ikiwezekana kikombe hiki kiniepuke; walakini si kama nitakavyo mimi, bali utakavyo wewe.” (Mathayo 26:39)
  • Isaya 55:8–9: “Mawazo yangu si mawazo yenu, wala njia zenu si njia zangu.”

Funzo:
Kuna wakati Mungu hatusikilizi kwa namna tunavyotaka, kwa sababu anajua kilicho bora zaidi kwa roho zetu.
Mungu hutupa kile tunachohitaji, si kila tunachotaka.
Hivyo, maombi kutojibiwa si dalili ya Mungu kutusahau — ni dalili kwamba mpango wake ni mkuu kuliko wetu.

4. NGUVU YA KRISTO HUKAMILIKA KATIKA UDAHAIFU

📖 2 Wakorintho 12:9–10 “Naye akaniambia, Neema yangu yakutosha; maana uweza wangu hutimilika katika udhaifu. Basi nitajisifia udhaifu wangu kwa furaha nyingi, ili uweza wa Kristo ukae juu yangu. Kwa hiyo napendezwa na udhaifu, na ufidhuli, na misiba, na adha, na shida, kwa ajili ya Kristo. Maana niwapo dhaifu ndipo nilipo na nguvu”

Paulo anasema: “Ndio maana napendezwa na udhaifu… kwa maana nikiwa dhaifu ndipo nilipo na nguvu.”  Hapa tunajifunza kanuni kuu ya kiroho:  Wakati tunapokuwa hatuna uwezo wetu, ndipo nguvu ya Mungu inapata nafasi ya kufanya kazi kikamilifu.

Maandiko ya Kusaidia:

  • Filipi 4:13: “Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu.”
  • Isaya 40:29–31: “Huwapa nguvu wazimiao, humwogezea nguvu yeye asiyekuwa na uwezo… watapanda kwa mbawa kama tai.”
  • Habakuki 3:17–19: Hata kama miti haitoi matunda, bado nitamshangilia Bwana — kwa maana “Bwana MUNGU ndiye nguvu yangu.”
  • Warumi 8:26 “Kadhalika Roho naye hutusaidia udhaifu wetu; kwa maana hatujui kuomba jinsi itupasavyo…” Udhaifu wa kiroho unamhitaji Roho Mtakatifu atupe nguvu ya kusimama na kuomba, maana bila Yeye tunashindwa.

Funzo:
Nguvu ya Mungu haionekani katika wakati wa amani tu, bali hasa katika nyakati za udhaifu, magumu, na majaribu.
Kama mafuta yanavyotoa mwanga yanapochomwa, vivyo hivyo nuru ya Kristo inang’aa zaidi ndani yetu tunapokuwa dhaifu.

5. MFANO WA WATU WA MUNGU WALIOONA NGUVU KATIKA UDAHAIFU

  • Musa: Alijiona si msemaji mzuri (Kutoka 4:10), lakini Mungu alimtumia kuwakomboa Israeli.
  • Gideoni: Alijiona duni (Waamuzi 6:15), lakini Mungu alimfanya shujaa.
  • Daudi: Alikuwa mchungaji mdogo, lakini Mungu alimfanya mfalme.
  • Petro: Alimkana Yesu mara tatu, lakini baadaye akawa mhubiri mwenye nguvu Mathayo 26:33-35, 69-75, Mdo 2:1-40

Funzo:
Mungu hapendi watu “wenye nguvu zao,” bali wale wanaotambua udhaifu wao na kumruhusu Kristo na Roho Mtakatifu kuwa nguvu yao.

HITIMISHO:- Udhaifu ni Wito wa Kutegemea Neema ya Mungu

📖 2 Wakorintho 12:9-10 “Neema yangu yakutosha; maana uweza wangu hutimilika katika udhaifu; Maana niwapo dhaifu ndipo nilipo na nguvu.”

Kwa hiyo, udhaifu ni nafasi ya Mungu kujionyesha mwenyewe kuwa Yeye ni Nguvu yetu.
Kadiri tunavyokuwa wanyonge, ndivyo Kristo anavyotukamilisha. Tunapokubali kwamba hatuwezi bila Mungu, ndipo anapoweza kufanya kazi kwa ukamilifu ndani yetu.

Imeandaliwa na : –

Mwl: Anselemi Mashimba Alloyce

Mwalimu wa Neno la Mungu

GREAT LOVE

John 15:13-15
[13]Greater love hath no man than this, that a man lay down his life for his friends.
[14]Ye are my friends, if ye do whatsoever I command you.
[15]Henceforth I call you not servants; for the servant knoweth not what his lord doeth: but I have called you friends; for all things that I have heard of my Father I have made known unto you.

IMANI NA FUNDISHO LA MITUME

Hivyo basi kama mtu akifundishwa kimakosa atajenga imani potofu; akifundishwa kwa usahihi atajenga imani njema/sahihi
Hapa ndipo palipopelekea kuanzisha fundisho.

A: IMANI NI NINI?
IMANI ni Kuwa na uhakika wa mambo/jambo unalolitarajia hasusani jambo lisiloonekana (Waebrania 11:1
Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo yasiyoonekana).
Imani mara zote huja kwa kusikia, au kufundishwa jambo fulani.
Warumi 10:17
Basi imani, chanzo chake ni kusikia; na kusikia huja kwa neno la Kristo.

Kabla ya kujibu tuangalie kwanza maana ya FUNDISHO
Fundisho katika AGANO JIPYA linabeba maana mbili
A). Tendo la Kufundisha 1Timotheo 4:13,16,5:17; 2Timotheo 3:10,16
B). Kile kinachofundishwa
Mathayo 15:9; 2Timotheo 4:13
Hivyo basi FUNDISHO ni maagizo, taarifa au maudhui yaliyomo kwenye kile kinachofundishwa.

B: FUNDISHO LA MITUME NI NINI?

FUNDISHO LA MITUME ni maagizo ya kwanza/mapema kabisa yaliyotolewa na mitume katika kanisa la kwanza
Fundisho la mitume liligawanyika katika maeneo makuu matatu kama ifuatavyo:-
1: YESU ndiye KRISTO. Matendo ya Mitume 9:22
Sauli akazidi kuwa hodari, akawatia fadhaa Wayahudi waliokaa Dameski, akithibitisha ya kuwa huyu ndiye Kristo.

Matendo ya Mitume 17:2, 3
Na Paulo, kama ilivyokuwa desturi yake, akaingia mle walimo, akahojiana nao kwa maneno ya maandiko sabato tatu, akiyafunua na kuwaeleza ya kwamba ilimpasa Kristo kuteswa, na kufufuka katika wafu; na ya kwamba, Yesu huyu ninayewapasha ninyi habari zake ndiye Kristo.

2: YESU amefufuka kutoka kwa wafu.
Matendo ya Mitume 1:2
hata siku ile alipochukuliwa juu, alipokuwa amekwisha kuwaagiza kwa Roho Mtakatifu wale mitume aliowachagua;

Matendo ya Mitume 1:3
wale aliowadhihirishia nafsi yake, kwa dalili nyingi, baada ya kuteswa kwake, ya kwamba yu hai, akiwatokea muda wa siku arobaini, na kuyanena mambo yaliyouhusu ufalme wa Mungu.

Matendo ya Mitume 1:22
kuanza tangu ubatizo wa Yohana, hata siku ile alipochukuliwa kwetu kwenda juu, inapasa mmoja wao awe shahidi wa kufufuka kwake pamoja nasi.

Matendo ya Mitume 2:2
Kukaja ghafula toka mbinguni uvumi kama uvumi wa upepo wa nguvu ukienda kasi, ukaijaza nyumba yote waliyokuwa wameketi.

Matendo ya Mitume 2:3
Kukawatokea ndimi zilizogawanyikana, kama ndimi za moto uliowakalia kila mmoja wao.

Matendo ya Mitume 2:23
mtu huyu alipotolewa kwa shauri la Mungu lililokusudiwa, na kwa kujua kwake tangu zamani, ninyi mkamsulibisha kwa mikono ya watu wabaya, mkamwua;

Matendo ya Mitume 2:24
ambaye Mungu alimfufua, akiufungua uchungu wa mauti, kwa sababu haikuwezekana ashikwe nao.

Matendo ya Mitume 2:2
Kukaja ghafula toka mbinguni uvumi kama uvumi wa upepo wa nguvu ukienda kasi, ukaijaza nyumba yote waliyokuwa wameketi.

Matendo ya Mitume 2:3
Kukawatokea ndimi zilizogawanyikana, kama ndimi za moto uliowakalia kila mmoja wao.

Matendo ya Mitume 2:23
mtu huyu alipotolewa kwa shauri la Mungu lililokusudiwa, na kwa kujua kwake tangu zamani, ninyi mkamsulibisha kwa mikono ya watu wabaya, mkamwua;

Matendo ya Mitume 2:24
ambaye Mungu alimfufua, akiufungua uchungu wa mauti, kwa sababu haikuwezekana ashikwe nao.

Matendo ya Mitume 2:32
Yesu huyo Mungu alimfufua, na sisi sote tu mashahidi wake.

3: WOKOVU inapatikana kupitia jina la Yesu kristo pekee. Matendo ya Mitume 4:12
Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo.

Matendo ya Mitume 3:16
Na kwa imani katika jina lake, jina lake limemtia nguvu mtu huyu mnayemwona na kumjua; na imani ile iliyo kwake yeye imempatia huyu uzima huu mkamilifu mbele yenu ninyi nyote.

Wakati wa kuhubiri fundisho hilo na kweli hizo tatu waliambatanisha na fundisho la IMANI KIYAHUDI ambayo msingi wake ni AGANO la Kale kuonyesha uvuvio na kutimizwa kwa agano la Kale. Soma mahubiri ya Petro, Stephano na Paulo ili uone namna ambavyo mtiririko ulikuwa na namna ambavyo agano la Kale limeungana na AGANO JIPYA
Matendo ya Mitume 2:14
Lakini Petro akasimama pamoja na wale kumi na mmoja, akapaza sauti yake, akawaambia, Enyi watu wa Uyahudi, na ninyi nyote mkaao Yerusalemu, lijueni jambo hili, mkasikilize maneno yangu.

Matendo ya Mitume 2:15
Sivyo mnavyodhani; watu hawa hawakulewa, kwa maana ni saa tatu ya mchana;

Matendo ya Mitume 2:16
lakini jambo hili ni lile lililonenwa kwa kinywa cha nabii Yoeli,

Matendo ya Mitume 2:17
Itakuwa siku za mwisho, asema Mungu, nitawamwagia watu wote Roho yangu, na wana wenu na binti zenu watatabiri; na vijana wenu wataona maono; na wazee wenu wataota ndoto.

Matendo ya Mitume 2:18
Naam, na siku zile nitawamwagia watumishi wangu wanaume na wanawake Roho yangu, nao watatabiri.

Matendo ya Mitume 2:19
Nami nitatoa ajabu katika mbingu juu, na ishara katika nchi chini, damu na moto, na mvuke wa moshi.

Matendo ya Mitume 2:20
Jua litageuka kuwa giza, na mwezi kuwa damu, kabla ya kuja ile siku ya Bwana iliyo kuu na iliyo dhahiri.

Matendo ya Mitume 2:21
Na itakuwa kila atakayeliitia jina la Bwana ataokolewa.

Matendo ya Mitume 2:22
Enyi waume wa Israeli, sikilizeni maneno haya: Yesu wa Nazareti, mtu aliyedhihirishwa kwenu na Mungu kwa miujiza na ajabu na ishara, ambazo Mungu alizifanya kwa mkono wake kati yenu, kama ninyi wenyewe mnavyojua;

Matendo ya Mitume 2:23
mtu huyu alipotolewa kwa shauri la Mungu lililokusudiwa, na kwa kujua kwake tangu zamani, ninyi mkamsulibisha kwa mikono ya watu wabaya, mkamwua;

Matendo ya Mitume 2:24
ambaye Mungu alimfufua, akiufungua uchungu wa mauti, kwa sababu haikuwezekana ashikwe nao.

Matendo ya Mitume 2:25
Maana Daudi ataja habari zake,
Nalimwona Bwana mbele yangu siku zote,
Kwa kuwa yuko upande wa mkono wangu wa kuume, nisitikisike.

Matendo ya Mitume 2:26
Kwa hiyo moyo wangu ukapendezewa,
ulimi wangu ukafurahi;
Tena mwili wangu nao utakaa katika matumaini.

Matendo ya Mitume 2:27
Kwa maana hutaiacha roho yangu katika kuzimu;
Wala hutamtoa Mtakatifu wako aone uharibifu.

Matendo ya Mitume 2:28
Umenijuvisha njia za uzima;
Utanijaza furaha kwa uso wako.

Matendo ya Mitume 2:29
Waume, ndugu zangu, mniwie radhi, niseme kwa ujasiri mbele yenu habari za baba yetu mkuu, Daudi, ya kuwa alifariki akazikwa, na kaburi lake liko kwetu hata leo.

Matendo ya Mitume 2:30
Basi kwa kuwa ni nabii, akijua ya kuwa Mungu amemwapia kwa kiapo, ya kwamba katika uzao wa viuno vyake atamketisha mmoja katika kiti chake cha enzi;

Matendo ya Mitume 2:31
yeye mwenyewe akitangulia kuyaona haya, alitaja habari za kufufuka kwake Kristo, ya kwamba roho yake haikuachwa kuzimu, wala mwili wake haukuona uharibifu.

Matendo ya Mitume 2:32
Yesu huyo Mungu alimfufua, na sisi sote tu mashahidi wake.

Matendo ya Mitume 2:33
Basi yeye, akiisha kupandishwa hata mkono wa kuume wa Mungu, na kupokea kwa Baba ile ahadi ya Roho Mtakatifu, amekimwaga kitu hiki mnachokiona sasa na kukisikia.

Matendo ya Mitume 2:34
Maana Daudi hakupanda mbinguni; bali yeye mwenyewe anasema,
Bwana alimwambia Bwana wangu,
Keti upande wa mkono wangu wa kuume.

Matendo ya Mitume 2:35
Hata nitakapowaweka adui zako chini ya miguu yako.

Matendo ya Mitume 2:36
Basi nyumba yote ya Israeli na wajue yakini ya kwamba Mungu amemfanya Yesu huyo mliyemsulibisha kuwa Bwana na Kristo.

(Soma pia Matendo ya mitume 5:29-32; 7:2-52)

Ndani ya fundisho la mitume kulikuwa na kweli kadha ambazo zilikuwa zikitiliwa mkazo; baadhi yake ni
1: Kristo alijitoa kufa msalabani ili kutimiza kusudi la Mungu la ukombozi.
Matendo ya Mitume 2:22
Enyi waume wa Israeli, sikilizeni maneno haya: Yesu wa Nazareti, mtu aliyedhihirishwa kwenu na Mungu kwa miujiza na ajabu na ishara, ambazo Mungu alizifanya kwa mkono wake kati yenu, kama ninyi wenyewe mnavyojua;

Matendo ya Mitume 2:23
mtu huyu alipotolewa kwa shauri la Mungu lililokusudiwa, na kwa kujua kwake tangu zamani, ninyi mkamsulibisha kwa mikono ya watu wabaya, mkamwua;

(Soma pia Matendo ya mitume 3:18-21)

2: YESU KRISTO yu hai alifufuka kutoka kwa wafu.
Matendo ya Mitume 2:24
ambaye Mungu alimfufua, akiufungua uchungu wa mauti, kwa sababu haikuwezekana ashikwe nao.

Matendo ya Mitume 2:25
Maana Daudi ataja habari zake,
Nalimwona Bwana mbele yangu siku zote,
Kwa kuwa yuko upande wa mkono wangu wa kuume, nisitikisike.

Matendo ya Mitume 2:26
Kwa hiyo moyo wangu ukapendezewa,
ulimi wangu ukafurahi;
Tena mwili wangu nao utakaa katika matumaini.

Matendo ya Mitume 2:27
Kwa maana hutaiacha roho yangu katika kuzimu;
Wala hutamtoa Mtakatifu wako aone uharibifu.

Matendo ya Mitume 2:28
Umenijuvisha njia za uzima;
Utanijaza furaha kwa uso wako.

Matendo ya Mitume 2:29
Waume, ndugu zangu, mniwie radhi, niseme kwa ujasiri mbele yenu habari za baba yetu mkuu, Daudi, ya kuwa alifariki akazikwa, na kaburi lake liko kwetu hata leo.

Matendo ya Mitume 2:30
Basi kwa kuwa ni nabii, akijua ya kuwa Mungu amemwapia kwa kiapo, ya kwamba katika uzao wa viuno vyake atamketisha mmoja katika kiti chake cha enzi;

Matendo ya Mitume 2:31
yeye mwenyewe akitangulia kuyaona haya, alitaja habari za kufufuka kwake Kristo, ya kwamba roho yake haikuachwa kuzimu, wala mwili wake haukuona uharibifu.

Matendo ya Mitume 2:32
Yesu huyo Mungu alimfufua, na sisi sote tu mashahidi wake.

3: Yesu Kristo yuko mkono wa kuume wa Mungu, mbinguni

Matendo ya Mitume 1:9
Akiisha kusema hayo, walipokuwa wakitazama, akainuliwa, wingu likampokea kutoka machoni pao.
Matendo ya Mitume 2:33
Basi yeye, akiisha kupandishwa hata mkono wa kuume wa Mungu, na kupokea kwa Baba ile ahadi ya Roho Mtakatifu, amekimwaga kitu hiki mnachokiona sasa na kukisikia.

Matendo ya Mitume 2:34
Maana Daudi hakupanda mbinguni; bali yeye mwenyewe anasema, Bwana alimwambia Bwana wangu, Keti upande wa mkono wangu wa kuume.

Matendo ya Mitume 2:35
Hata nitakapowaweka adui zako chini ya miguu yako.

4: YESU ni BWANA na ndiye KRISTO
Matendo ya Mitume 2:36
Basi nyumba yote ya Israeli na wajue yakini ya kwamba Mungu amemfanya Yesu huyo mliyemsulibisha kuwa BWANA na KRISTO.

5: Imani katika jina la Yesu Kristo, ina nguvu na huleta uponyaji, wa kimwili na kiroho
Matendo ya Mitume 3:16
Na kwa imani katika jina lake, jina lake limemtia nguvu mtu huyu mnayemwona na kumjua; na imani ile iliyo kwake yeye imempatia huyu uzima huu mkamilifu mbele yenu ninyi nyote.

Matendo ya Mitume 3:17
Basi sasa, ndugu, najua ya kuwa mliyatenda haya kwa kutokujua kwenu, kama na wakuu wenu walivyotenda.

Matendo ya Mitume 3:18
Lakini mambo yale aliyohubiri Mungu tangu zamani kwa kinywa cha manabii wake wote, ya kwamba Kristo wake atateswa, ameyatimiza hivyo.

Matendo ya Mitume 3:19
Tubuni basi, mrejee, ili dhambi zenu zifutwe, zipate kuja nyakati za kuburudishwa kwa kuwako kwake Bwana;

Matendo ya Mitume 3:20
apate kumtuma Kristo Yesu mliyewekewa tangu zamani;
Matendo ya Mitume 9:34
Petro akamwambia, Ainea, Yesu Kristo akuponya; ondoka, ujitandikie. Mara akaondoka.

Matendo ya Mitume 10:43
Huyo manabii wote humshuhudia, ya kwamba kwa jina lake kila amwaminiye atapata ondoleo la dhambi.

Tangu kipindi cha MITUME kulikuwa na upotoshaji na kupigwa vita sana dhidi ya imani na matumizi ya jina la Yesu kristo
(Soma, Matendo ya mitume 4:13-22; 5:27-29,40)

Hata sasa katika zama zetu wako wahubiri, manabii, mitume, waalimu na wachungaji ambao kwa namna moja ama nyingine wanajaribu kuonyesha kwamba jina la Yesu kristo halitoshi ndiyo maana wanaweka viambata ambavyo wanaweka kama vile chumvi, mafuta, vitambaa, picha zao, n.k, mambo hayo ni kuturudisha agano la Kale yaani torati ambapo AGANO LA KALE ni kivuli. Kwa nini kujitia kwenye kongwa tena na kutumia kitu mbadala wakati kitu halisi kipo?
Wakolosai 2:13
Na ninyi mlipokuwa mmekufa kwa sababu ya makosa yenu na kutokutahiriwa kwa mwili wenu, aliwafanya hai pamoja naye, akiisha kutusamehe makosa yote;

Wakolosai 2:14
akiisha kuifuta ile hati iliyoandikwa ya kutushitaki kwa hukumu zake, iliyokuwa na uadui kwetu; akaiondoa isiwepo tena, akaigongomea msalabani;

Wakolosai 2:15
akiisha kuzivua enzi na mamlaka, na kuzifanya kuwa mkogo kwa ujasiri, akizishangilia katika msalaba huo.

Wakolosai 2:16
Basi, mtu asiwahukumu ninyi katika vyakula au vinywaji, au kwa sababu ya sikukuu au mwandamo wa mwezi, au sabato;

Wakolosai 2:17
mambo hayo ni kivuli cha mambo yajayo; bali mwili ni wa Kristo.

6: Mamlaka ya Yesu Kristo kusamehe dhambi
Matendo ya Mitume 5:31
Mtu huyo Mungu amemtukuza kwa mkono wake wa kuume, awe Mkuu na Mwokozi, awape Waisraeli toba na msamaha wa dhambi.

7: Ujazo na utendaji wa Roho Mtakatifu
Matendo ya Mitume 8:14
Na mitume waliokuwako Yerusalemu, waliposikia ya kwamba Samaria imelikubali neno la Mungu, wakawapelekea Petro na Yohana;

Matendo ya Mitume 8:15
ambao waliposhuka, wakawaombea wampokee Roho Mtakatifu;

Matendo ya Mitume 8:16
kwa maana bado hajawashukia hata mmoja wao, ila wamebatizwa tu kwa jina lake Bwana Yesu.

Matendo ya Mitume 8:17
Ndipo wakaweka mikono yao juu yao, nao wakampokea Roho Mtakatifu.

(Soma, Matendo ya mitume 8:29; 10:44-47)
8: Ubatizo wa maji mengi
Matendo ya Mitume 8:35
Filipo akafunua kinywa chake, naye, akianza kwa andiko lilo hilo, akamhubiri habari njema za Yesu.

Matendo ya Mitume 8:36
Wakawa wakiendelea njiani, wakafika mahali penye maji; yule towashi akasema, Tazama, maji haya; ni nini kinachonizuia nisibatizwe? [

Matendo ya Mitume 8:37
Filipo akasema, Ukiamini kwa moyo wako wote, inawezekana. Akajibu, akanena, Naamini ya kwamba Yesu Kristo ndiye Mwana wa Mungu.]

Matendo ya Mitume 8:38
Akaamuru lile gari lisimame; wakatelemka wote wawili majini, Filipo na yule towashi; naye akambatiza.

Matendo ya Mitume 8:39
Kisha, walipopanda kutoka majini, Roho wa Bwana akamnyakua Filipo, yule towashi asimwone tena; basi alikwenda zake akifurahi.

Matendo ya Mitume 10:47
Ni nani awezaye kuzuia maji, hawa wasibatizwe, watu waliopokea Roho Mtakatifu vile vile kama sisi?

Matendo ya Mitume 10:48
Akaamuru wabatizwe kwa Jina lake Yesu Kristo. Ndipo wakamsihi azidi kukaa siku kadha wa kadha.

9: Tumaini la mbingu mpya na nchi mpya
2 Petro 3:13
Lakini, kama ilivyo ahadi yake, mnatazamia mbingu mpya na nchi mpya, ambayo haki yakaa ndani yake.

Hilo ndilo fundisho la mitume ambalo kanisa la leo limejengwa juu yake
Mathayo 16:16
Simoni Petro akajibu akasema, Wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai.

Mathayo 16:17
Yesu akajibu, akamwambia, Heri wewe Simoni Bar-yona; kwa kuwa mwili na damu havikukufunulia hili, bali Baba yangu aliye mbinguni.

Mathayo 16:18
Nami nakuambia, Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; wala milango ya kuzimu haitalishinda.

Mathayo 16:19
Nami nitakupa wewe funguo za ufalme wa mbinguni; na lo lote utakalolifunga duniani, litakuwa limefungwa mbinguni; na lo lote utakalolifungua duniani, litakuwa limefunguliwa mbinguni.
1 Petro 2:4
Mmwendee yeye, jiwe lililo hai, lililokataliwa na wanadamu, bali kwa Mungu ni teule, lenye heshima.

1 Petro 2:5
Ninyi nanyi, kama mawe yaliyo hai, mmejengwa mwe nyumba ya Roho, ukuhani mtakatifu, mtoe dhabihu za roho, zinazokubaliwa na Mungu, kwa njia ya Yesu Kristo.

1 Petro 2:6
Kwa kuwa imeandikwa katika maandiko
Tazama, naweka katika Sayuni jiwe kuu la pembeni, teule, lenye heshima,
Na kila amwaminiye hatatahayarika.

1 Petro 2:7
Basi, heshima hii ni kwenu ninyi mnaoamini. Bali kwao wasioamini,
Jiwe walilolikataa waashi,
Limekuwa jiwe kuu la pembeni.

1 Petro 2:8
Tena,
Jiwe la kujikwaza mguu, na mwamba wa kuangusha.
Kwa maana hujikwaza kwa neno lile, wasiliamini, nao waliwekwa kusudi wapate hayo.

1 Petro 2:9
Bali ninyi ni mzao mteule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu wa milki ya Mungu, mpate kuzitangaza fadhili zake yeye aliyewaita mtoke gizani mkaingie katika nuru yake ya ajabu;

1 Petro 2:10
ninyi mliokuwa kwanza si taifa, bali sasa ni taifa la Mungu; mliokuwa hamkupata rehema, bali sasa mmepata rehema.

Mwamba ni YESU KRISTO hivyo kanisa limejengwa juu ya Kristo

IMANI NA FUNDISHO LA MITUME

A: IMANI NI NINI?
IMANI ni Kuwa na uhakika wa mambo/jambo unalolitarajia hasusani jambo lisiloonekana (Waebrania 11:1
Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo yasiyoonekana).
Imani mara zote huja kwa kusikia, au kufundishwa jambo fulani.
Warumi 10:17
Basi imani, chanzo chake ni kusikia; na kusikia huja kwa neno la Kristo.

Hivyo basi kama mtu akifundishwa kimakosa atajenga imani potofu; akifundishwa kwa usahihi atajenga imani njema/sahihi
Hapa ndipo palipopelekea kuanzisha fundisho.

B: FUNDISHO LA MITUME NI NINI?

Kabla ya kujibu tuangalie kwanza maana ya FUNDISHO
Fundisho katika AGANO JIPYA linabeba maana mbili
A). Tendo la Kufundisha 1Timotheo 4:13,16,5:17; 2Timotheo 3:10,16
B). Kile kinachofundishwa
Mathayo 15:9; 2Timotheo 4:13
Hivyo basi FUNDISHO ni maagizo, taarifa au maudhui yaliyomo kwenye kile kinachofundishwa.

FUNDISHO LA MITUME ni maagizo ya kwanza/mapema kabisa yaliyotolewa na mitume katika kanisa la kwanza
Fundisho la mitume liligawanyika katika maeneo makuu matatu kama ifuatavyo:-
1: YESU ndiye KRISTO. Matendo ya Mitume 9:22
Sauli akazidi kuwa hodari, akawatia fadhaa Wayahudi waliokaa Dameski, akithibitisha ya kuwa huyu ndiye Kristo.

Matendo ya Mitume 17:2, 3
Na Paulo, kama ilivyokuwa desturi yake, akaingia mle walimo, akahojiana nao kwa maneno ya maandiko sabato tatu, akiyafunua na kuwaeleza ya kwamba ilimpasa Kristo kuteswa, na kufufuka katika wafu; na ya kwamba, Yesu huyu ninayewapasha ninyi habari zake ndiye Kristo.

2: YESU amefufuka kutoka kwa wafu.
Matendo ya Mitume 1:2
hata siku ile alipochukuliwa juu, alipokuwa amekwisha kuwaagiza kwa Roho Mtakatifu wale mitume aliowachagua;

Matendo ya Mitume 1:3
wale aliowadhihirishia nafsi yake, kwa dalili nyingi, baada ya kuteswa kwake, ya kwamba yu hai, akiwatokea muda wa siku arobaini, na kuyanena mambo yaliyouhusu ufalme wa Mungu.

Matendo ya Mitume 1:22
kuanza tangu ubatizo wa Yohana, hata siku ile alipochukuliwa kwetu kwenda juu, inapasa mmoja wao awe shahidi wa kufufuka kwake pamoja nasi.

Matendo ya Mitume 2:2
Kukaja ghafula toka mbinguni uvumi kama uvumi wa upepo wa nguvu ukienda kasi, ukaijaza nyumba yote waliyokuwa wameketi.

Matendo ya Mitume 2:3
Kukawatokea ndimi zilizogawanyikana, kama ndimi za moto uliowakalia kila mmoja wao.

Matendo ya Mitume 2:23
mtu huyu alipotolewa kwa shauri la Mungu lililokusudiwa, na kwa kujua kwake tangu zamani, ninyi mkamsulibisha kwa mikono ya watu wabaya, mkamwua;

Matendo ya Mitume 2:24
ambaye Mungu alimfufua, akiufungua uchungu wa mauti, kwa sababu haikuwezekana ashikwe nao.

Matendo ya Mitume 2:2
Kukaja ghafula toka mbinguni uvumi kama uvumi wa upepo wa nguvu ukienda kasi, ukaijaza nyumba yote waliyokuwa wameketi.

Matendo ya Mitume 2:3
Kukawatokea ndimi zilizogawanyikana, kama ndimi za moto uliowakalia kila mmoja wao.

Matendo ya Mitume 2:23
mtu huyu alipotolewa kwa shauri la Mungu lililokusudiwa, na kwa kujua kwake tangu zamani, ninyi mkamsulibisha kwa mikono ya watu wabaya, mkamwua;

Matendo ya Mitume 2:24
ambaye Mungu alimfufua, akiufungua uchungu wa mauti, kwa sababu haikuwezekana ashikwe nao.

Matendo ya Mitume 2:32
Yesu huyo Mungu alimfufua, na sisi sote tu mashahidi wake.

3: WOKOVU inapatikana kupitia jina la Yesu kristo pekee. Matendo ya Mitume 4:12
Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo.

Matendo ya Mitume 3:16
Na kwa imani katika jina lake, jina lake limemtia nguvu mtu huyu mnayemwona na kumjua; na imani ile iliyo kwake yeye imempatia huyu uzima huu mkamilifu mbele yenu ninyi nyote.

Wakati wa kuhubiri fundisho hilo na kweli hizo tatu waliambatanisha na fundisho la IMANI KIYAHUDI ambayo msingi wake ni AGANO la Kale kuonyesha uvuvio na kutimizwa kwa agano la Kale. Soma mahubiri ya Petro, Stephano na Paulo ili uone namna ambavyo mtiririko ulikuwa na namna ambavyo agano la Kale limeungana na AGANO JIPYA
Matendo ya Mitume 2:14
Lakini Petro akasimama pamoja na wale kumi na mmoja, akapaza sauti yake, akawaambia, Enyi watu wa Uyahudi, na ninyi nyote mkaao Yerusalemu, lijueni jambo hili, mkasikilize maneno yangu.

Matendo ya Mitume 2:15
Sivyo mnavyodhani; watu hawa hawakulewa, kwa maana ni saa tatu ya mchana;

Matendo ya Mitume 2:16
lakini jambo hili ni lile lililonenwa kwa kinywa cha nabii Yoeli,

Matendo ya Mitume 2:17
Itakuwa siku za mwisho, asema Mungu, nitawamwagia watu wote Roho yangu, na wana wenu na binti zenu watatabiri; na vijana wenu wataona maono; na wazee wenu wataota ndoto.

Matendo ya Mitume 2:18
Naam, na siku zile nitawamwagia watumishi wangu wanaume na wanawake Roho yangu, nao watatabiri.

Matendo ya Mitume 2:19
Nami nitatoa ajabu katika mbingu juu, na ishara katika nchi chini, damu na moto, na mvuke wa moshi.

Matendo ya Mitume 2:20
Jua litageuka kuwa giza, na mwezi kuwa damu, kabla ya kuja ile siku ya Bwana iliyo kuu na iliyo dhahiri.

Matendo ya Mitume 2:21
Na itakuwa kila atakayeliitia jina la Bwana ataokolewa.

Matendo ya Mitume 2:22
Enyi waume wa Israeli, sikilizeni maneno haya: Yesu wa Nazareti, mtu aliyedhihirishwa kwenu na Mungu kwa miujiza na ajabu na ishara, ambazo Mungu alizifanya kwa mkono wake kati yenu, kama ninyi wenyewe mnavyojua;

Matendo ya Mitume 2:23
mtu huyu alipotolewa kwa shauri la Mungu lililokusudiwa, na kwa kujua kwake tangu zamani, ninyi mkamsulibisha kwa mikono ya watu wabaya, mkamwua;

Matendo ya Mitume 2:24
ambaye Mungu alimfufua, akiufungua uchungu wa mauti, kwa sababu haikuwezekana ashikwe nao.

Matendo ya Mitume 2:25
Maana Daudi ataja habari zake,
Nalimwona Bwana mbele yangu siku zote,
Kwa kuwa yuko upande wa mkono wangu wa kuume, nisitikisike.

Matendo ya Mitume 2:26
Kwa hiyo moyo wangu ukapendezewa,
ulimi wangu ukafurahi;
Tena mwili wangu nao utakaa katika matumaini.

Matendo ya Mitume 2:27
Kwa maana hutaiacha roho yangu katika kuzimu;
Wala hutamtoa Mtakatifu wako aone uharibifu.

Matendo ya Mitume 2:28
Umenijuvisha njia za uzima;
Utanijaza furaha kwa uso wako.

Matendo ya Mitume 2:29
Waume, ndugu zangu, mniwie radhi, niseme kwa ujasiri mbele yenu habari za baba yetu mkuu, Daudi, ya kuwa alifariki akazikwa, na kaburi lake liko kwetu hata leo.

Matendo ya Mitume 2:30
Basi kwa kuwa ni nabii, akijua ya kuwa Mungu amemwapia kwa kiapo, ya kwamba katika uzao wa viuno vyake atamketisha mmoja katika kiti chake cha enzi;

Matendo ya Mitume 2:31
yeye mwenyewe akitangulia kuyaona haya, alitaja habari za kufufuka kwake Kristo, ya kwamba roho yake haikuachwa kuzimu, wala mwili wake haukuona uharibifu.

Matendo ya Mitume 2:32
Yesu huyo Mungu alimfufua, na sisi sote tu mashahidi wake.

Matendo ya Mitume 2:33
Basi yeye, akiisha kupandishwa hata mkono wa kuume wa Mungu, na kupokea kwa Baba ile ahadi ya Roho Mtakatifu, amekimwaga kitu hiki mnachokiona sasa na kukisikia.

Matendo ya Mitume 2:34
Maana Daudi hakupanda mbinguni; bali yeye mwenyewe anasema,
Bwana alimwambia Bwana wangu,
Keti upande wa mkono wangu wa kuume.

Matendo ya Mitume 2:35
Hata nitakapowaweka adui zako chini ya miguu yako.

Matendo ya Mitume 2:36
Basi nyumba yote ya Israeli na wajue yakini ya kwamba Mungu amemfanya Yesu huyo mliyemsulibisha kuwa Bwana na Kristo.

(Soma pia Matendo ya mitume 5:29-32; 7:2-52)

Ndani ya fundisho la mitume kulikuwa na kweli kadha ambazo zilikuwa zikitiliwa mkazo; baadhi yake ni
1: Kristo alijitoa kufa msalabani ili kutimiza kusudi la Mungu la ukombozi.
Matendo ya Mitume 2:22
Enyi waume wa Israeli, sikilizeni maneno haya: Yesu wa Nazareti, mtu aliyedhihirishwa kwenu na Mungu kwa miujiza na ajabu na ishara, ambazo Mungu alizifanya kwa mkono wake kati yenu, kama ninyi wenyewe mnavyojua;

Matendo ya Mitume 2:23
mtu huyu alipotolewa kwa shauri la Mungu lililokusudiwa, na kwa kujua kwake tangu zamani, ninyi mkamsulibisha kwa mikono ya watu wabaya, mkamwua;

(Soma pia Matendo ya mitume 3:18-21)

2: YESU KRISTO yu hai alifufuka kutoka kwa wafu.
Matendo ya Mitume 2:24
ambaye Mungu alimfufua, akiufungua uchungu wa mauti, kwa sababu haikuwezekana ashikwe nao.

Matendo ya Mitume 2:25
Maana Daudi ataja habari zake,
Nalimwona Bwana mbele yangu siku zote,
Kwa kuwa yuko upande wa mkono wangu wa kuume, nisitikisike.

Matendo ya Mitume 2:26
Kwa hiyo moyo wangu ukapendezewa,
ulimi wangu ukafurahi;
Tena mwili wangu nao utakaa katika matumaini.

Matendo ya Mitume 2:27
Kwa maana hutaiacha roho yangu katika kuzimu;
Wala hutamtoa Mtakatifu wako aone uharibifu.

Matendo ya Mitume 2:28
Umenijuvisha njia za uzima;
Utanijaza furaha kwa uso wako.

Matendo ya Mitume 2:29
Waume, ndugu zangu, mniwie radhi, niseme kwa ujasiri mbele yenu habari za baba yetu mkuu, Daudi, ya kuwa alifariki akazikwa, na kaburi lake liko kwetu hata leo.

Matendo ya Mitume 2:30
Basi kwa kuwa ni nabii, akijua ya kuwa Mungu amemwapia kwa kiapo, ya kwamba katika uzao wa viuno vyake atamketisha mmoja katika kiti chake cha enzi;

Matendo ya Mitume 2:31
yeye mwenyewe akitangulia kuyaona haya, alitaja habari za kufufuka kwake Kristo, ya kwamba roho yake haikuachwa kuzimu, wala mwili wake haukuona uharibifu.

Matendo ya Mitume 2:32
Yesu huyo Mungu alimfufua, na sisi sote tu mashahidi wake.

3: Yesu Kristo yuko mkono wa kuume wa Mungu, mbinguni

Matendo ya Mitume 1:9
Akiisha kusema hayo, walipokuwa wakitazama, akainuliwa, wingu likampokea kutoka machoni pao.
Matendo ya Mitume 2:33
Basi yeye, akiisha kupandishwa hata mkono wa kuume wa Mungu, na kupokea kwa Baba ile ahadi ya Roho Mtakatifu, amekimwaga kitu hiki mnachokiona sasa na kukisikia.

Matendo ya Mitume 2:34
Maana Daudi hakupanda mbinguni; bali yeye mwenyewe anasema, Bwana alimwambia Bwana wangu, Keti upande wa mkono wangu wa kuume.

Matendo ya Mitume 2:35
Hata nitakapowaweka adui zako chini ya miguu yako.

4: YESU ni BWANA na ndiye KRISTO
Matendo ya Mitume 2:36
Basi nyumba yote ya Israeli na wajue yakini ya kwamba Mungu amemfanya Yesu huyo mliyemsulibisha kuwa BWANA na KRISTO.

5: Imani katika jina la Yesu Kristo, ina nguvu na huleta uponyaji, wa kimwili na kiroho
Matendo ya Mitume 3:16
Na kwa imani katika jina lake, jina lake limemtia nguvu mtu huyu mnayemwona na kumjua; na imani ile iliyo kwake yeye imempatia huyu uzima huu mkamilifu mbele yenu ninyi nyote.

Matendo ya Mitume 3:17
Basi sasa, ndugu, najua ya kuwa mliyatenda haya kwa kutokujua kwenu, kama na wakuu wenu walivyotenda.

Matendo ya Mitume 3:18
Lakini mambo yale aliyohubiri Mungu tangu zamani kwa kinywa cha manabii wake wote, ya kwamba Kristo wake atateswa, ameyatimiza hivyo.

Matendo ya Mitume 3:19
Tubuni basi, mrejee, ili dhambi zenu zifutwe, zipate kuja nyakati za kuburudishwa kwa kuwako kwake Bwana;

Matendo ya Mitume 3:20
apate kumtuma Kristo Yesu mliyewekewa tangu zamani;
Matendo ya Mitume 9:34
Petro akamwambia, Ainea, Yesu Kristo akuponya; ondoka, ujitandikie. Mara akaondoka.

Matendo ya Mitume 10:43
Huyo manabii wote humshuhudia, ya kwamba kwa jina lake kila amwaminiye atapata ondoleo la dhambi.

Tangu kipindi cha MITUME kulikuwa na upotoshaji na kupigwa vita sana dhidi ya imani na matumizi ya jina la Yesu kristo
(Soma, Matendo ya mitume 4:13-22; 5:27-29,40)

Hata sasa katika zama zetu wako wahubiri, manabii, mitume, waalimu na wachungaji ambao kwa namna moja ama nyingine wanajaribu kuonyesha kwamba jina la Yesu kristo halitoshi ndiyo maana wanaweka viambata ambavyo wanaweka kama vile chumvi, mafuta, vitambaa, picha zao, n.k, mambo hayo ni kuturudisha agano la Kale yaani torati ambapo AGANO LA KALE ni kivuli. Kwa nini kujitia kwenye kongwa tena na kutumia kitu mbadala wakati kitu halisi kipo?
Wakolosai 2:13
Na ninyi mlipokuwa mmekufa kwa sababu ya makosa yenu na kutokutahiriwa kwa mwili wenu, aliwafanya hai pamoja naye, akiisha kutusamehe makosa yote;

Wakolosai 2:14
akiisha kuifuta ile hati iliyoandikwa ya kutushitaki kwa hukumu zake, iliyokuwa na uadui kwetu; akaiondoa isiwepo tena, akaigongomea msalabani;

Wakolosai 2:15
akiisha kuzivua enzi na mamlaka, na kuzifanya kuwa mkogo kwa ujasiri, akizishangilia katika msalaba huo.

Wakolosai 2:16
Basi, mtu asiwahukumu ninyi katika vyakula au vinywaji, au kwa sababu ya sikukuu au mwandamo wa mwezi, au sabato;

Wakolosai 2:17
mambo hayo ni kivuli cha mambo yajayo; bali mwili ni wa Kristo.

6: Mamlaka ya Yesu Kristo kusamehe dhambi
Matendo ya Mitume 5:31
Mtu huyo Mungu amemtukuza kwa mkono wake wa kuume, awe Mkuu na Mwokozi, awape Waisraeli toba na msamaha wa dhambi.

7: Ujazo na utendaji wa Roho Mtakatifu
Matendo ya Mitume 8:14
Na mitume waliokuwako Yerusalemu, waliposikia ya kwamba Samaria imelikubali neno la Mungu, wakawapelekea Petro na Yohana;

Matendo ya Mitume 8:15
ambao waliposhuka, wakawaombea wampokee Roho Mtakatifu;

Matendo ya Mitume 8:16
kwa maana bado hajawashukia hata mmoja wao, ila wamebatizwa tu kwa jina lake Bwana Yesu.

Matendo ya Mitume 8:17
Ndipo wakaweka mikono yao juu yao, nao wakampokea Roho Mtakatifu.

(Soma, Matendo ya mitume 8:29; 10:44-47)
8: Ubatizo wa maji mengi
Matendo ya Mitume 8:35
Filipo akafunua kinywa chake, naye, akianza kwa andiko lilo hilo, akamhubiri habari njema za Yesu.

Matendo ya Mitume 8:36
Wakawa wakiendelea njiani, wakafika mahali penye maji; yule towashi akasema, Tazama, maji haya; ni nini kinachonizuia nisibatizwe? [

Matendo ya Mitume 8:37
Filipo akasema, Ukiamini kwa moyo wako wote, inawezekana. Akajibu, akanena, Naamini ya kwamba Yesu Kristo ndiye Mwana wa Mungu.]

Matendo ya Mitume 8:38
Akaamuru lile gari lisimame; wakatelemka wote wawili majini, Filipo na yule towashi; naye akambatiza.

Matendo ya Mitume 8:39
Kisha, walipopanda kutoka majini, Roho wa Bwana akamnyakua Filipo, yule towashi asimwone tena; basi alikwenda zake akifurahi.

Matendo ya Mitume 10:47
Ni nani awezaye kuzuia maji, hawa wasibatizwe, watu waliopokea Roho Mtakatifu vile vile kama sisi?

Matendo ya Mitume 10:48
Akaamuru wabatizwe kwa Jina lake Yesu Kristo. Ndipo wakamsihi azidi kukaa siku kadha wa kadha.

9: Tumaini la mbingu mpya na nchi mpya
2 Petro 3:13
Lakini, kama ilivyo ahadi yake, mnatazamia mbingu mpya na nchi mpya, ambayo haki yakaa ndani yake.

Hilo ndilo fundisho la mitume ambalo kanisa la leo limejengwa juu yake
Mathayo 16:16
Simoni Petro akajibu akasema, Wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai.

Mathayo 16:17
Yesu akajibu, akamwambia, Heri wewe Simoni Bar-yona; kwa kuwa mwili na damu havikukufunulia hili, bali Baba yangu aliye mbinguni.

Mathayo 16:18
Nami nakuambia, Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; wala milango ya kuzimu haitalishinda.

Mathayo 16:19
Nami nitakupa wewe funguo za ufalme wa mbinguni; na lo lote utakalolifunga duniani, litakuwa limefungwa mbinguni; na lo lote utakalolifungua duniani, litakuwa limefunguliwa mbinguni.
1 Petro 2:4
Mmwendee yeye, jiwe lililo hai, lililokataliwa na wanadamu, bali kwa Mungu ni teule, lenye heshima.

1 Petro 2:5
Ninyi nanyi, kama mawe yaliyo hai, mmejengwa mwe nyumba ya Roho, ukuhani mtakatifu, mtoe dhabihu za roho, zinazokubaliwa na Mungu, kwa njia ya Yesu Kristo.

1 Petro 2:6
Kwa kuwa imeandikwa katika maandiko
Tazama, naweka katika Sayuni jiwe kuu la pembeni, teule, lenye heshima,
Na kila amwaminiye hatatahayarika.

1 Petro 2:7
Basi, heshima hii ni kwenu ninyi mnaoamini. Bali kwao wasioamini,
Jiwe walilolikataa waashi,
Limekuwa jiwe kuu la pembeni.

1 Petro 2:8
Tena,
Jiwe la kujikwaza mguu, na mwamba wa kuangusha.
Kwa maana hujikwaza kwa neno lile, wasiliamini, nao waliwekwa kusudi wapate hayo.

1 Petro 2:9
Bali ninyi ni mzao mteule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu wa milki ya Mungu, mpate kuzitangaza fadhili zake yeye aliyewaita mtoke gizani mkaingie katika nuru yake ya ajabu;

1 Petro 2:10
ninyi mliokuwa kwanza si taifa, bali sasa ni taifa la Mungu; mliokuwa hamkupata rehema, bali sasa mmepata rehema.

Mwamba ni YESU KRISTO hivyo kanisa limejengwa juu ya Kristo