MAADILI NA NIDHAMU YA KIROHO KWA MKRISTO

Somo: Maadili na Nidhamu ya Kiroho kwa Mkristo

Kichwa kidogo: Kuishi Maisha Safi Katika Kristo

Maandiko ya Kifungu Kikuu: 1 Wakorintho 6:18-20; 1 Wakorintho 10:31; 1 Wakorintho 9:24-27

Ujumbe wa Somo:
Mkristo anatakiwa kuishi maisha ya maadili mema na nidhamu ya kiroho kwa sababu mwili wake ni hekalu la Roho Mtakatifu, na kila tendo lake linaathiri ushuhuda wake na utukufu wa Mungu.


Hoja Kuu 1: Mwili wa Mkristo ni Hekalu la Roho Mtakatifu

Andiko: 1 Wakorintho 6:19-20 – “Je! Hamjui kwamba miili yenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, mliopewa na Mungu, na kwamba hamjawiwa wenyewe? Kwa maana mmelipwa kwa gharama; kwa hiyo mtii Mungu katika miili yenu.”

Maelezo:

  • Mwili wa Mkristo si mali ya kawaida; ni hekalu la Mungu.
  • Hii inamaanisha kuwa kila tendo la kimwili au kiroho linapaswa kuonyesha heshima na hofu ya Mungu.
  • Dhambi za kimwili au tamaa zisizo na nidhamu zinaharibu hekalu hili na kushusha heshima ya imani.

Mfano:

  • Kila kitendo tunachokifanya, kama kutumia maneno, kushirikiana na wengine, au hata kula na kunywa, kinaweza kuwa kitendo cha heshima kwa Mungu au kidhambi. Mfano moyo kulemewa na ulafi, ulevi na masubufu ya dunia Luka 21:34, 35, War 13:13

Hoja Kuu 2: Epuka Dhambi na Ndoto/tamaa za Mwili

Andiko: 1 Wakorintho 6:18 – “Epuka uzinzi. Kila dhambi ya mtu yeyote inatoka nje ya mwili; lakini yule anaye kufanya uzinzi anakiuka mwili wake.”

Maelezo:

  • Uzinzi ni mfano wa tamaa za mwili zisizo na nidhamu.
  • Dhambi ya kimwili ina madhara ya kiroho na mara nyingi inaathiri maisha yote ya Mkristo, ikiwa ni pamoja na ushuhuda wake mbele ya wengine. Mfano Mfalme Daudi kitendo cha kuzini na Mke wa Uria kilisababisha matatizo mengi mno kwake, familia yake na Taifa kwa ujumla 2 Sam 12:1-14
  • Nidhamu ya kiroho inamaanisha kudhibiti tamaa na kuishi kwa heshima ya Mungu, kwa kuzingatia mipaka ya Biblia tikiwezeshwa na neema ya Mungu. War 13:11-14, Tit 2:11-13

Hoja Kuu 3: Kila Kitendo Kifanyike Kwa Utukufu wa Mungu

Andiko: 1 Wakorintho 10:31 – “Kwa hiyo, mkile, mkinywa, au mkifanya kitu kingine, fanyeni yote kwa utukufu wa Mungu.”

Maelezo:

  • Nidhamu ya kiroho inajumuisha kufanya kila jambo kwa heshima na utukufu wa Mungu, si kwa maslahi yetu binafsi au kujipendekeza kwa watu. Miili yetu itumike kwa utukufu wa Bwana
  • Hii inahusisha mambo madogo na makubwa: maneno, matendo, kazi, hata starehe.
  • Mkristo aliye na nidhamu ya kiroho anafanya kila jambo kwa nia ya kumtukuza Mungu. 1 Kor 6:12-17, Wakolosai 1:10, 3:23, 24

Hoja Kuu 4: Nidhamu ya Kiroho inahitaji Ushirikiano wa Akili na Mwili

Andiko: 1 Wakorintho 9:24-27 – “Hamjui kwamba katika mbio zote wanabashiri wote wanakimbia, lakini mmoja anapata tuzo? Kimbieni ili mupate. Kila mtu anayekimbia anadhibiti mwili wake; ili si kama atakuwa akimwaga kwa bure. Nimiye kama asiye na nidhamu, mimi nawafunga mwili wangu na kuwafanya wanyenyeke, nisipokuwa mimi mwenyewe nikipotea.”

Maelezo:

  • Paulo anafananisha maisha ya kiroho na mbio za riadha. Mkristo anapaswa kudhibiti tamaa, mazoea mabaya, na tabia zisizo za kiroho.
  • Nidhamu ya kiroho inahitaji mazoezi makali, kusali, kujizuia, na kuzingatia mafundisho ya Biblia. 1Tim 4:7,8; Ebra 12:11
  • Hii inatupa ushindi wa kiroho na kuimarisha ushuhuda wa Kikristo.

Hoja Kuu 5: Matokeo ya Maadili na Nidhamu

Maandiko: 1 Wakorintho 10:12-13 – “Kwa hiyo, mtu yeyote akidhani kuwa amesimama, aangalie asipate kuanguka. Hakika hakuna majaribu yaliyokukuta isipokuwa yale ya kawaida kwa wanadamu; lakini Mungu ni mwaminifu, hatakuruhusu mtihani ukuzidi uwezo wenu, bali atatupatia njia ya kutoka ili tuweze kustahimili.”

Maelezo:

  • Nidhamu ya kiroho hutoa mkingo wa kuepuka dhambi na kuishi maisha ya ushuhuda.
  • Mungu hutoa nguvu na njia ya kustahimili kila jaribu.
  • Mkristo aliye na nidhamu ya kiroho ana amani ya moyo na heshima kwa Mungu na watu. War 5: 1

Hitimisho

  • Maadili na nidhamu ya kiroho ni msingi wa maisha ya Kikristo.
  • Mwili wetu ni hekalu la Roho, matendo yetu lazima yawe kwa utukufu wa Mungu.
  • Nidhamu inahitaji mazoezi ya kiroho, kujizuia, na kushirikiana na Mungu kila siku.
  • Kwa kuishi maisha yenye maadili na nidhamu ya kiroho, Mkristo anaweza kushuhudia imani yake kwa nguvu, na kufurahia tumaini la milele.

Imeandaliwa na Mwalimu Anselemi Mashimba Alloyce

WhatsApp +255747 251 929

NGUVU YA MUNGU KATIKA UDHAIFU WETU

SOMO: NGUVU YA KRISTO KATIKA UDHAIFU WETU

Andiko Kuu: 2 Wakorintho 12:1–10. “Neema yangu yakutosha; kwa maana nguvu yangu hukamilika katika udhaifu.” (2 Wakorintho 12:9)

UTANGULIZI

Wapendwa katika Kristo Yesu, maisha ya Mkristo siyo safari ya raha na mafanikio ya kila siku, bali ni njia yenye majaribu, udhaifu, na maumivu, ambamo Mungu anajifunua kwa namna ya ajabu.
Mtume Paulo anatufundisha kwamba udhaifu si kushindwa, bali ni mwangalizo wa nafasi ya nguvu ya Mungu kufanya kazi ndani yetu.

MAANA YA UDHAIFU KIBIBLIA.

Udhaifu ni Kukosa Uwezo wa Kujitegemea Bila Mungu

Biblia inafundisha kwamba udhaifu wa kweli ni kutambua kwamba bila Mungu hatuwezi chochote.

📖 Yohana 15:5 “Mimi ni mzabibu, ninyi matawi; akaaye ndani yangu, nami ndani yake, huyo huzaa sana; kwa maana pasipo mimi ninyi hamuwezi kufanya neno lo lote.”

Hivyo udhaifu sio tu hali ya kushindwa, bali ni kutambua uhalisia wetu wa kibinadamu — kwamba nguvu, hekima, na uhai wote hutoka kwa Mungu. Na kutambua udhaifu huleta unyenyekevu ndani yetu kwa Mungu wetu

Kwa Kigiriki neno linalotumika katika 2 Wakorintho 12:9 ni “astheneia” likimaanisha: kutokuwa na nguvu, kutokuwa na uwezo, au hali ya udhaifu wa kimwili, kiroho, au kihisia.

1. MUNGU HUFUNUA SIRI KWA WANYENYEKEVU

📖 2 Wakorintho 12:1–4. Paulo alipata ufunuo wa mbinguni ya tatu, lakini hakujivuna — alikaa mnyenyekevu. Mungu alijua moyo wake na alihakikisha Paulo anabaki katika unyenyekevu kwa kumpa “mwiba katika mwili.”

Maandiko ya Kusaidia:

  • Yakobo 4:6: “Mungu huwapinga wenye kiburi, bali huwapa neema wanyenyekevu.”
  • Mithali 11:2: “Kujivuna huleta aibu, bali hekima iko kwa wanyenyekevu.”

Funzo:
Watu wengi wanapobarikiwa na ufunuo, au karama, huanza kujisifu kana kwamba ni kwa uwezo wao. Mungu, kwa hekima yake, huwaruhusu kupitia mambo yanayowakumbusha kuwa bado ni wanadamu. Hivyo, unyenyekevu ni kinga dhidi ya kuanguka kiroho.

2. MWIBA KATIKA MWILI NI SEHEMU YA SAFARI YA IMANI

📖 2 Wakorintho 12:7–8. Paulo alipewa “mwiba” ili asijiinuwe kupita kiasi. Haijulikani hasa ulikuwa ni ugonjwa, mateso, au mapambano ya kiroho — lakini ilikuwa ni hali iliyomtesa sana.

Maandiko ya Kusaidia:

  • Ayubu 23:10: “Lakini ajua njia nitembeayo; akishanijaribu, nitatoka kama dhahabu.”
  • Zaburi 119:71: “Imenifaa kuteseka, ili nipate kujifunza maagizo yako.”
  • Warumi 8:28: “Na tunajua ya kuwa katika mambo yote Mungu hufanya kazi pamoja na wale wampendao kwa mema.”

Funzo:
Kuna mateso ambayo Mungu huruhusu si kwa adhabu, bali kwa mafunzo ya kiroho.
Mwiba unatusaidia tusisahau tunamtegemea Mungu, si sisi wenyewe.
Kama vile dhahabu inavyosafishwa kwa moto, vivyo hivyo imani yetu inakua kupitia majaribu.

3. MAOMBI YASIYOJIBIWA KWA NJIA TUNAYOTARAJIA: Maombi yakizanayo na kusudi la Mungu

📖 2 Wakorintho 12:8. Paulo aliomba mara tatu Bwana auondoe ule mwiba, lakini Mungu hakufanya hivyo. Badala yake alimjibu: “Neema yangu yakutosha.”

Maandiko ya Kusaidia:

  • Yesu mwenyewe aliomba: “Baba, ikiwezekana kikombe hiki kiniepuke; walakini si kama nitakavyo mimi, bali utakavyo wewe.” (Mathayo 26:39)
  • Isaya 55:8–9: “Mawazo yangu si mawazo yenu, wala njia zenu si njia zangu.”

Funzo:
Kuna wakati Mungu hatusikilizi kwa namna tunavyotaka, kwa sababu anajua kilicho bora zaidi kwa roho zetu.
Mungu hutupa kile tunachohitaji, si kila tunachotaka.
Hivyo, maombi kutojibiwa si dalili ya Mungu kutusahau — ni dalili kwamba mpango wake ni mkuu kuliko wetu.

4. NGUVU YA KRISTO HUKAMILIKA KATIKA UDAHAIFU

📖 2 Wakorintho 12:9–10 “Naye akaniambia, Neema yangu yakutosha; maana uweza wangu hutimilika katika udhaifu. Basi nitajisifia udhaifu wangu kwa furaha nyingi, ili uweza wa Kristo ukae juu yangu. Kwa hiyo napendezwa na udhaifu, na ufidhuli, na misiba, na adha, na shida, kwa ajili ya Kristo. Maana niwapo dhaifu ndipo nilipo na nguvu”

Paulo anasema: “Ndio maana napendezwa na udhaifu… kwa maana nikiwa dhaifu ndipo nilipo na nguvu.”  Hapa tunajifunza kanuni kuu ya kiroho:  Wakati tunapokuwa hatuna uwezo wetu, ndipo nguvu ya Mungu inapata nafasi ya kufanya kazi kikamilifu.

Maandiko ya Kusaidia:

  • Filipi 4:13: “Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu.”
  • Isaya 40:29–31: “Huwapa nguvu wazimiao, humwogezea nguvu yeye asiyekuwa na uwezo… watapanda kwa mbawa kama tai.”
  • Habakuki 3:17–19: Hata kama miti haitoi matunda, bado nitamshangilia Bwana — kwa maana “Bwana MUNGU ndiye nguvu yangu.”
  • Warumi 8:26 “Kadhalika Roho naye hutusaidia udhaifu wetu; kwa maana hatujui kuomba jinsi itupasavyo…” Udhaifu wa kiroho unamhitaji Roho Mtakatifu atupe nguvu ya kusimama na kuomba, maana bila Yeye tunashindwa.

Funzo:
Nguvu ya Mungu haionekani katika wakati wa amani tu, bali hasa katika nyakati za udhaifu, magumu, na majaribu.
Kama mafuta yanavyotoa mwanga yanapochomwa, vivyo hivyo nuru ya Kristo inang’aa zaidi ndani yetu tunapokuwa dhaifu.

5. MFANO WA WATU WA MUNGU WALIOONA NGUVU KATIKA UDAHAIFU

  • Musa: Alijiona si msemaji mzuri (Kutoka 4:10), lakini Mungu alimtumia kuwakomboa Israeli.
  • Gideoni: Alijiona duni (Waamuzi 6:15), lakini Mungu alimfanya shujaa.
  • Daudi: Alikuwa mchungaji mdogo, lakini Mungu alimfanya mfalme.
  • Petro: Alimkana Yesu mara tatu, lakini baadaye akawa mhubiri mwenye nguvu Mathayo 26:33-35, 69-75, Mdo 2:1-40

Funzo:
Mungu hapendi watu “wenye nguvu zao,” bali wale wanaotambua udhaifu wao na kumruhusu Kristo na Roho Mtakatifu kuwa nguvu yao.

HITIMISHO:- Udhaifu ni Wito wa Kutegemea Neema ya Mungu

📖 2 Wakorintho 12:9-10 “Neema yangu yakutosha; maana uweza wangu hutimilika katika udhaifu; Maana niwapo dhaifu ndipo nilipo na nguvu.”

Kwa hiyo, udhaifu ni nafasi ya Mungu kujionyesha mwenyewe kuwa Yeye ni Nguvu yetu.
Kadiri tunavyokuwa wanyonge, ndivyo Kristo anavyotukamilisha. Tunapokubali kwamba hatuwezi bila Mungu, ndipo anapoweza kufanya kazi kwa ukamilifu ndani yetu.

Imeandaliwa na : –

Mwl: Anselemi Mashimba Alloyce

Mwalimu wa Neno la Mungu

GREAT LOVE

John 15:13-15
[13]Greater love hath no man than this, that a man lay down his life for his friends.
[14]Ye are my friends, if ye do whatsoever I command you.
[15]Henceforth I call you not servants; for the servant knoweth not what his lord doeth: but I have called you friends; for all things that I have heard of my Father I have made known unto you.

IMANI NA FUNDISHO LA MITUME

Hivyo basi kama mtu akifundishwa kimakosa atajenga imani potofu; akifundishwa kwa usahihi atajenga imani njema/sahihi
Hapa ndipo palipopelekea kuanzisha fundisho.

A: IMANI NI NINI?
IMANI ni Kuwa na uhakika wa mambo/jambo unalolitarajia hasusani jambo lisiloonekana (Waebrania 11:1
Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo yasiyoonekana).
Imani mara zote huja kwa kusikia, au kufundishwa jambo fulani.
Warumi 10:17
Basi imani, chanzo chake ni kusikia; na kusikia huja kwa neno la Kristo.

Kabla ya kujibu tuangalie kwanza maana ya FUNDISHO
Fundisho katika AGANO JIPYA linabeba maana mbili
A). Tendo la Kufundisha 1Timotheo 4:13,16,5:17; 2Timotheo 3:10,16
B). Kile kinachofundishwa
Mathayo 15:9; 2Timotheo 4:13
Hivyo basi FUNDISHO ni maagizo, taarifa au maudhui yaliyomo kwenye kile kinachofundishwa.

B: FUNDISHO LA MITUME NI NINI?

FUNDISHO LA MITUME ni maagizo ya kwanza/mapema kabisa yaliyotolewa na mitume katika kanisa la kwanza
Fundisho la mitume liligawanyika katika maeneo makuu matatu kama ifuatavyo:-
1: YESU ndiye KRISTO. Matendo ya Mitume 9:22
Sauli akazidi kuwa hodari, akawatia fadhaa Wayahudi waliokaa Dameski, akithibitisha ya kuwa huyu ndiye Kristo.

Matendo ya Mitume 17:2, 3
Na Paulo, kama ilivyokuwa desturi yake, akaingia mle walimo, akahojiana nao kwa maneno ya maandiko sabato tatu, akiyafunua na kuwaeleza ya kwamba ilimpasa Kristo kuteswa, na kufufuka katika wafu; na ya kwamba, Yesu huyu ninayewapasha ninyi habari zake ndiye Kristo.

2: YESU amefufuka kutoka kwa wafu.
Matendo ya Mitume 1:2
hata siku ile alipochukuliwa juu, alipokuwa amekwisha kuwaagiza kwa Roho Mtakatifu wale mitume aliowachagua;

Matendo ya Mitume 1:3
wale aliowadhihirishia nafsi yake, kwa dalili nyingi, baada ya kuteswa kwake, ya kwamba yu hai, akiwatokea muda wa siku arobaini, na kuyanena mambo yaliyouhusu ufalme wa Mungu.

Matendo ya Mitume 1:22
kuanza tangu ubatizo wa Yohana, hata siku ile alipochukuliwa kwetu kwenda juu, inapasa mmoja wao awe shahidi wa kufufuka kwake pamoja nasi.

Matendo ya Mitume 2:2
Kukaja ghafula toka mbinguni uvumi kama uvumi wa upepo wa nguvu ukienda kasi, ukaijaza nyumba yote waliyokuwa wameketi.

Matendo ya Mitume 2:3
Kukawatokea ndimi zilizogawanyikana, kama ndimi za moto uliowakalia kila mmoja wao.

Matendo ya Mitume 2:23
mtu huyu alipotolewa kwa shauri la Mungu lililokusudiwa, na kwa kujua kwake tangu zamani, ninyi mkamsulibisha kwa mikono ya watu wabaya, mkamwua;

Matendo ya Mitume 2:24
ambaye Mungu alimfufua, akiufungua uchungu wa mauti, kwa sababu haikuwezekana ashikwe nao.

Matendo ya Mitume 2:2
Kukaja ghafula toka mbinguni uvumi kama uvumi wa upepo wa nguvu ukienda kasi, ukaijaza nyumba yote waliyokuwa wameketi.

Matendo ya Mitume 2:3
Kukawatokea ndimi zilizogawanyikana, kama ndimi za moto uliowakalia kila mmoja wao.

Matendo ya Mitume 2:23
mtu huyu alipotolewa kwa shauri la Mungu lililokusudiwa, na kwa kujua kwake tangu zamani, ninyi mkamsulibisha kwa mikono ya watu wabaya, mkamwua;

Matendo ya Mitume 2:24
ambaye Mungu alimfufua, akiufungua uchungu wa mauti, kwa sababu haikuwezekana ashikwe nao.

Matendo ya Mitume 2:32
Yesu huyo Mungu alimfufua, na sisi sote tu mashahidi wake.

3: WOKOVU inapatikana kupitia jina la Yesu kristo pekee. Matendo ya Mitume 4:12
Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo.

Matendo ya Mitume 3:16
Na kwa imani katika jina lake, jina lake limemtia nguvu mtu huyu mnayemwona na kumjua; na imani ile iliyo kwake yeye imempatia huyu uzima huu mkamilifu mbele yenu ninyi nyote.

Wakati wa kuhubiri fundisho hilo na kweli hizo tatu waliambatanisha na fundisho la IMANI KIYAHUDI ambayo msingi wake ni AGANO la Kale kuonyesha uvuvio na kutimizwa kwa agano la Kale. Soma mahubiri ya Petro, Stephano na Paulo ili uone namna ambavyo mtiririko ulikuwa na namna ambavyo agano la Kale limeungana na AGANO JIPYA
Matendo ya Mitume 2:14
Lakini Petro akasimama pamoja na wale kumi na mmoja, akapaza sauti yake, akawaambia, Enyi watu wa Uyahudi, na ninyi nyote mkaao Yerusalemu, lijueni jambo hili, mkasikilize maneno yangu.

Matendo ya Mitume 2:15
Sivyo mnavyodhani; watu hawa hawakulewa, kwa maana ni saa tatu ya mchana;

Matendo ya Mitume 2:16
lakini jambo hili ni lile lililonenwa kwa kinywa cha nabii Yoeli,

Matendo ya Mitume 2:17
Itakuwa siku za mwisho, asema Mungu, nitawamwagia watu wote Roho yangu, na wana wenu na binti zenu watatabiri; na vijana wenu wataona maono; na wazee wenu wataota ndoto.

Matendo ya Mitume 2:18
Naam, na siku zile nitawamwagia watumishi wangu wanaume na wanawake Roho yangu, nao watatabiri.

Matendo ya Mitume 2:19
Nami nitatoa ajabu katika mbingu juu, na ishara katika nchi chini, damu na moto, na mvuke wa moshi.

Matendo ya Mitume 2:20
Jua litageuka kuwa giza, na mwezi kuwa damu, kabla ya kuja ile siku ya Bwana iliyo kuu na iliyo dhahiri.

Matendo ya Mitume 2:21
Na itakuwa kila atakayeliitia jina la Bwana ataokolewa.

Matendo ya Mitume 2:22
Enyi waume wa Israeli, sikilizeni maneno haya: Yesu wa Nazareti, mtu aliyedhihirishwa kwenu na Mungu kwa miujiza na ajabu na ishara, ambazo Mungu alizifanya kwa mkono wake kati yenu, kama ninyi wenyewe mnavyojua;

Matendo ya Mitume 2:23
mtu huyu alipotolewa kwa shauri la Mungu lililokusudiwa, na kwa kujua kwake tangu zamani, ninyi mkamsulibisha kwa mikono ya watu wabaya, mkamwua;

Matendo ya Mitume 2:24
ambaye Mungu alimfufua, akiufungua uchungu wa mauti, kwa sababu haikuwezekana ashikwe nao.

Matendo ya Mitume 2:25
Maana Daudi ataja habari zake,
Nalimwona Bwana mbele yangu siku zote,
Kwa kuwa yuko upande wa mkono wangu wa kuume, nisitikisike.

Matendo ya Mitume 2:26
Kwa hiyo moyo wangu ukapendezewa,
ulimi wangu ukafurahi;
Tena mwili wangu nao utakaa katika matumaini.

Matendo ya Mitume 2:27
Kwa maana hutaiacha roho yangu katika kuzimu;
Wala hutamtoa Mtakatifu wako aone uharibifu.

Matendo ya Mitume 2:28
Umenijuvisha njia za uzima;
Utanijaza furaha kwa uso wako.

Matendo ya Mitume 2:29
Waume, ndugu zangu, mniwie radhi, niseme kwa ujasiri mbele yenu habari za baba yetu mkuu, Daudi, ya kuwa alifariki akazikwa, na kaburi lake liko kwetu hata leo.

Matendo ya Mitume 2:30
Basi kwa kuwa ni nabii, akijua ya kuwa Mungu amemwapia kwa kiapo, ya kwamba katika uzao wa viuno vyake atamketisha mmoja katika kiti chake cha enzi;

Matendo ya Mitume 2:31
yeye mwenyewe akitangulia kuyaona haya, alitaja habari za kufufuka kwake Kristo, ya kwamba roho yake haikuachwa kuzimu, wala mwili wake haukuona uharibifu.

Matendo ya Mitume 2:32
Yesu huyo Mungu alimfufua, na sisi sote tu mashahidi wake.

Matendo ya Mitume 2:33
Basi yeye, akiisha kupandishwa hata mkono wa kuume wa Mungu, na kupokea kwa Baba ile ahadi ya Roho Mtakatifu, amekimwaga kitu hiki mnachokiona sasa na kukisikia.

Matendo ya Mitume 2:34
Maana Daudi hakupanda mbinguni; bali yeye mwenyewe anasema,
Bwana alimwambia Bwana wangu,
Keti upande wa mkono wangu wa kuume.

Matendo ya Mitume 2:35
Hata nitakapowaweka adui zako chini ya miguu yako.

Matendo ya Mitume 2:36
Basi nyumba yote ya Israeli na wajue yakini ya kwamba Mungu amemfanya Yesu huyo mliyemsulibisha kuwa Bwana na Kristo.

(Soma pia Matendo ya mitume 5:29-32; 7:2-52)

Ndani ya fundisho la mitume kulikuwa na kweli kadha ambazo zilikuwa zikitiliwa mkazo; baadhi yake ni
1: Kristo alijitoa kufa msalabani ili kutimiza kusudi la Mungu la ukombozi.
Matendo ya Mitume 2:22
Enyi waume wa Israeli, sikilizeni maneno haya: Yesu wa Nazareti, mtu aliyedhihirishwa kwenu na Mungu kwa miujiza na ajabu na ishara, ambazo Mungu alizifanya kwa mkono wake kati yenu, kama ninyi wenyewe mnavyojua;

Matendo ya Mitume 2:23
mtu huyu alipotolewa kwa shauri la Mungu lililokusudiwa, na kwa kujua kwake tangu zamani, ninyi mkamsulibisha kwa mikono ya watu wabaya, mkamwua;

(Soma pia Matendo ya mitume 3:18-21)

2: YESU KRISTO yu hai alifufuka kutoka kwa wafu.
Matendo ya Mitume 2:24
ambaye Mungu alimfufua, akiufungua uchungu wa mauti, kwa sababu haikuwezekana ashikwe nao.

Matendo ya Mitume 2:25
Maana Daudi ataja habari zake,
Nalimwona Bwana mbele yangu siku zote,
Kwa kuwa yuko upande wa mkono wangu wa kuume, nisitikisike.

Matendo ya Mitume 2:26
Kwa hiyo moyo wangu ukapendezewa,
ulimi wangu ukafurahi;
Tena mwili wangu nao utakaa katika matumaini.

Matendo ya Mitume 2:27
Kwa maana hutaiacha roho yangu katika kuzimu;
Wala hutamtoa Mtakatifu wako aone uharibifu.

Matendo ya Mitume 2:28
Umenijuvisha njia za uzima;
Utanijaza furaha kwa uso wako.

Matendo ya Mitume 2:29
Waume, ndugu zangu, mniwie radhi, niseme kwa ujasiri mbele yenu habari za baba yetu mkuu, Daudi, ya kuwa alifariki akazikwa, na kaburi lake liko kwetu hata leo.

Matendo ya Mitume 2:30
Basi kwa kuwa ni nabii, akijua ya kuwa Mungu amemwapia kwa kiapo, ya kwamba katika uzao wa viuno vyake atamketisha mmoja katika kiti chake cha enzi;

Matendo ya Mitume 2:31
yeye mwenyewe akitangulia kuyaona haya, alitaja habari za kufufuka kwake Kristo, ya kwamba roho yake haikuachwa kuzimu, wala mwili wake haukuona uharibifu.

Matendo ya Mitume 2:32
Yesu huyo Mungu alimfufua, na sisi sote tu mashahidi wake.

3: Yesu Kristo yuko mkono wa kuume wa Mungu, mbinguni

Matendo ya Mitume 1:9
Akiisha kusema hayo, walipokuwa wakitazama, akainuliwa, wingu likampokea kutoka machoni pao.
Matendo ya Mitume 2:33
Basi yeye, akiisha kupandishwa hata mkono wa kuume wa Mungu, na kupokea kwa Baba ile ahadi ya Roho Mtakatifu, amekimwaga kitu hiki mnachokiona sasa na kukisikia.

Matendo ya Mitume 2:34
Maana Daudi hakupanda mbinguni; bali yeye mwenyewe anasema, Bwana alimwambia Bwana wangu, Keti upande wa mkono wangu wa kuume.

Matendo ya Mitume 2:35
Hata nitakapowaweka adui zako chini ya miguu yako.

4: YESU ni BWANA na ndiye KRISTO
Matendo ya Mitume 2:36
Basi nyumba yote ya Israeli na wajue yakini ya kwamba Mungu amemfanya Yesu huyo mliyemsulibisha kuwa BWANA na KRISTO.

5: Imani katika jina la Yesu Kristo, ina nguvu na huleta uponyaji, wa kimwili na kiroho
Matendo ya Mitume 3:16
Na kwa imani katika jina lake, jina lake limemtia nguvu mtu huyu mnayemwona na kumjua; na imani ile iliyo kwake yeye imempatia huyu uzima huu mkamilifu mbele yenu ninyi nyote.

Matendo ya Mitume 3:17
Basi sasa, ndugu, najua ya kuwa mliyatenda haya kwa kutokujua kwenu, kama na wakuu wenu walivyotenda.

Matendo ya Mitume 3:18
Lakini mambo yale aliyohubiri Mungu tangu zamani kwa kinywa cha manabii wake wote, ya kwamba Kristo wake atateswa, ameyatimiza hivyo.

Matendo ya Mitume 3:19
Tubuni basi, mrejee, ili dhambi zenu zifutwe, zipate kuja nyakati za kuburudishwa kwa kuwako kwake Bwana;

Matendo ya Mitume 3:20
apate kumtuma Kristo Yesu mliyewekewa tangu zamani;
Matendo ya Mitume 9:34
Petro akamwambia, Ainea, Yesu Kristo akuponya; ondoka, ujitandikie. Mara akaondoka.

Matendo ya Mitume 10:43
Huyo manabii wote humshuhudia, ya kwamba kwa jina lake kila amwaminiye atapata ondoleo la dhambi.

Tangu kipindi cha MITUME kulikuwa na upotoshaji na kupigwa vita sana dhidi ya imani na matumizi ya jina la Yesu kristo
(Soma, Matendo ya mitume 4:13-22; 5:27-29,40)

Hata sasa katika zama zetu wako wahubiri, manabii, mitume, waalimu na wachungaji ambao kwa namna moja ama nyingine wanajaribu kuonyesha kwamba jina la Yesu kristo halitoshi ndiyo maana wanaweka viambata ambavyo wanaweka kama vile chumvi, mafuta, vitambaa, picha zao, n.k, mambo hayo ni kuturudisha agano la Kale yaani torati ambapo AGANO LA KALE ni kivuli. Kwa nini kujitia kwenye kongwa tena na kutumia kitu mbadala wakati kitu halisi kipo?
Wakolosai 2:13
Na ninyi mlipokuwa mmekufa kwa sababu ya makosa yenu na kutokutahiriwa kwa mwili wenu, aliwafanya hai pamoja naye, akiisha kutusamehe makosa yote;

Wakolosai 2:14
akiisha kuifuta ile hati iliyoandikwa ya kutushitaki kwa hukumu zake, iliyokuwa na uadui kwetu; akaiondoa isiwepo tena, akaigongomea msalabani;

Wakolosai 2:15
akiisha kuzivua enzi na mamlaka, na kuzifanya kuwa mkogo kwa ujasiri, akizishangilia katika msalaba huo.

Wakolosai 2:16
Basi, mtu asiwahukumu ninyi katika vyakula au vinywaji, au kwa sababu ya sikukuu au mwandamo wa mwezi, au sabato;

Wakolosai 2:17
mambo hayo ni kivuli cha mambo yajayo; bali mwili ni wa Kristo.

6: Mamlaka ya Yesu Kristo kusamehe dhambi
Matendo ya Mitume 5:31
Mtu huyo Mungu amemtukuza kwa mkono wake wa kuume, awe Mkuu na Mwokozi, awape Waisraeli toba na msamaha wa dhambi.

7: Ujazo na utendaji wa Roho Mtakatifu
Matendo ya Mitume 8:14
Na mitume waliokuwako Yerusalemu, waliposikia ya kwamba Samaria imelikubali neno la Mungu, wakawapelekea Petro na Yohana;

Matendo ya Mitume 8:15
ambao waliposhuka, wakawaombea wampokee Roho Mtakatifu;

Matendo ya Mitume 8:16
kwa maana bado hajawashukia hata mmoja wao, ila wamebatizwa tu kwa jina lake Bwana Yesu.

Matendo ya Mitume 8:17
Ndipo wakaweka mikono yao juu yao, nao wakampokea Roho Mtakatifu.

(Soma, Matendo ya mitume 8:29; 10:44-47)
8: Ubatizo wa maji mengi
Matendo ya Mitume 8:35
Filipo akafunua kinywa chake, naye, akianza kwa andiko lilo hilo, akamhubiri habari njema za Yesu.

Matendo ya Mitume 8:36
Wakawa wakiendelea njiani, wakafika mahali penye maji; yule towashi akasema, Tazama, maji haya; ni nini kinachonizuia nisibatizwe? [

Matendo ya Mitume 8:37
Filipo akasema, Ukiamini kwa moyo wako wote, inawezekana. Akajibu, akanena, Naamini ya kwamba Yesu Kristo ndiye Mwana wa Mungu.]

Matendo ya Mitume 8:38
Akaamuru lile gari lisimame; wakatelemka wote wawili majini, Filipo na yule towashi; naye akambatiza.

Matendo ya Mitume 8:39
Kisha, walipopanda kutoka majini, Roho wa Bwana akamnyakua Filipo, yule towashi asimwone tena; basi alikwenda zake akifurahi.

Matendo ya Mitume 10:47
Ni nani awezaye kuzuia maji, hawa wasibatizwe, watu waliopokea Roho Mtakatifu vile vile kama sisi?

Matendo ya Mitume 10:48
Akaamuru wabatizwe kwa Jina lake Yesu Kristo. Ndipo wakamsihi azidi kukaa siku kadha wa kadha.

9: Tumaini la mbingu mpya na nchi mpya
2 Petro 3:13
Lakini, kama ilivyo ahadi yake, mnatazamia mbingu mpya na nchi mpya, ambayo haki yakaa ndani yake.

Hilo ndilo fundisho la mitume ambalo kanisa la leo limejengwa juu yake
Mathayo 16:16
Simoni Petro akajibu akasema, Wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai.

Mathayo 16:17
Yesu akajibu, akamwambia, Heri wewe Simoni Bar-yona; kwa kuwa mwili na damu havikukufunulia hili, bali Baba yangu aliye mbinguni.

Mathayo 16:18
Nami nakuambia, Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; wala milango ya kuzimu haitalishinda.

Mathayo 16:19
Nami nitakupa wewe funguo za ufalme wa mbinguni; na lo lote utakalolifunga duniani, litakuwa limefungwa mbinguni; na lo lote utakalolifungua duniani, litakuwa limefunguliwa mbinguni.
1 Petro 2:4
Mmwendee yeye, jiwe lililo hai, lililokataliwa na wanadamu, bali kwa Mungu ni teule, lenye heshima.

1 Petro 2:5
Ninyi nanyi, kama mawe yaliyo hai, mmejengwa mwe nyumba ya Roho, ukuhani mtakatifu, mtoe dhabihu za roho, zinazokubaliwa na Mungu, kwa njia ya Yesu Kristo.

1 Petro 2:6
Kwa kuwa imeandikwa katika maandiko
Tazama, naweka katika Sayuni jiwe kuu la pembeni, teule, lenye heshima,
Na kila amwaminiye hatatahayarika.

1 Petro 2:7
Basi, heshima hii ni kwenu ninyi mnaoamini. Bali kwao wasioamini,
Jiwe walilolikataa waashi,
Limekuwa jiwe kuu la pembeni.

1 Petro 2:8
Tena,
Jiwe la kujikwaza mguu, na mwamba wa kuangusha.
Kwa maana hujikwaza kwa neno lile, wasiliamini, nao waliwekwa kusudi wapate hayo.

1 Petro 2:9
Bali ninyi ni mzao mteule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu wa milki ya Mungu, mpate kuzitangaza fadhili zake yeye aliyewaita mtoke gizani mkaingie katika nuru yake ya ajabu;

1 Petro 2:10
ninyi mliokuwa kwanza si taifa, bali sasa ni taifa la Mungu; mliokuwa hamkupata rehema, bali sasa mmepata rehema.

Mwamba ni YESU KRISTO hivyo kanisa limejengwa juu ya Kristo

IMANI NA FUNDISHO LA MITUME

A: IMANI NI NINI?
IMANI ni Kuwa na uhakika wa mambo/jambo unalolitarajia hasusani jambo lisiloonekana (Waebrania 11:1
Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo yasiyoonekana).
Imani mara zote huja kwa kusikia, au kufundishwa jambo fulani.
Warumi 10:17
Basi imani, chanzo chake ni kusikia; na kusikia huja kwa neno la Kristo.

Hivyo basi kama mtu akifundishwa kimakosa atajenga imani potofu; akifundishwa kwa usahihi atajenga imani njema/sahihi
Hapa ndipo palipopelekea kuanzisha fundisho.

B: FUNDISHO LA MITUME NI NINI?

Kabla ya kujibu tuangalie kwanza maana ya FUNDISHO
Fundisho katika AGANO JIPYA linabeba maana mbili
A). Tendo la Kufundisha 1Timotheo 4:13,16,5:17; 2Timotheo 3:10,16
B). Kile kinachofundishwa
Mathayo 15:9; 2Timotheo 4:13
Hivyo basi FUNDISHO ni maagizo, taarifa au maudhui yaliyomo kwenye kile kinachofundishwa.

FUNDISHO LA MITUME ni maagizo ya kwanza/mapema kabisa yaliyotolewa na mitume katika kanisa la kwanza
Fundisho la mitume liligawanyika katika maeneo makuu matatu kama ifuatavyo:-
1: YESU ndiye KRISTO. Matendo ya Mitume 9:22
Sauli akazidi kuwa hodari, akawatia fadhaa Wayahudi waliokaa Dameski, akithibitisha ya kuwa huyu ndiye Kristo.

Matendo ya Mitume 17:2, 3
Na Paulo, kama ilivyokuwa desturi yake, akaingia mle walimo, akahojiana nao kwa maneno ya maandiko sabato tatu, akiyafunua na kuwaeleza ya kwamba ilimpasa Kristo kuteswa, na kufufuka katika wafu; na ya kwamba, Yesu huyu ninayewapasha ninyi habari zake ndiye Kristo.

2: YESU amefufuka kutoka kwa wafu.
Matendo ya Mitume 1:2
hata siku ile alipochukuliwa juu, alipokuwa amekwisha kuwaagiza kwa Roho Mtakatifu wale mitume aliowachagua;

Matendo ya Mitume 1:3
wale aliowadhihirishia nafsi yake, kwa dalili nyingi, baada ya kuteswa kwake, ya kwamba yu hai, akiwatokea muda wa siku arobaini, na kuyanena mambo yaliyouhusu ufalme wa Mungu.

Matendo ya Mitume 1:22
kuanza tangu ubatizo wa Yohana, hata siku ile alipochukuliwa kwetu kwenda juu, inapasa mmoja wao awe shahidi wa kufufuka kwake pamoja nasi.

Matendo ya Mitume 2:2
Kukaja ghafula toka mbinguni uvumi kama uvumi wa upepo wa nguvu ukienda kasi, ukaijaza nyumba yote waliyokuwa wameketi.

Matendo ya Mitume 2:3
Kukawatokea ndimi zilizogawanyikana, kama ndimi za moto uliowakalia kila mmoja wao.

Matendo ya Mitume 2:23
mtu huyu alipotolewa kwa shauri la Mungu lililokusudiwa, na kwa kujua kwake tangu zamani, ninyi mkamsulibisha kwa mikono ya watu wabaya, mkamwua;

Matendo ya Mitume 2:24
ambaye Mungu alimfufua, akiufungua uchungu wa mauti, kwa sababu haikuwezekana ashikwe nao.

Matendo ya Mitume 2:2
Kukaja ghafula toka mbinguni uvumi kama uvumi wa upepo wa nguvu ukienda kasi, ukaijaza nyumba yote waliyokuwa wameketi.

Matendo ya Mitume 2:3
Kukawatokea ndimi zilizogawanyikana, kama ndimi za moto uliowakalia kila mmoja wao.

Matendo ya Mitume 2:23
mtu huyu alipotolewa kwa shauri la Mungu lililokusudiwa, na kwa kujua kwake tangu zamani, ninyi mkamsulibisha kwa mikono ya watu wabaya, mkamwua;

Matendo ya Mitume 2:24
ambaye Mungu alimfufua, akiufungua uchungu wa mauti, kwa sababu haikuwezekana ashikwe nao.

Matendo ya Mitume 2:32
Yesu huyo Mungu alimfufua, na sisi sote tu mashahidi wake.

3: WOKOVU inapatikana kupitia jina la Yesu kristo pekee. Matendo ya Mitume 4:12
Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo.

Matendo ya Mitume 3:16
Na kwa imani katika jina lake, jina lake limemtia nguvu mtu huyu mnayemwona na kumjua; na imani ile iliyo kwake yeye imempatia huyu uzima huu mkamilifu mbele yenu ninyi nyote.

Wakati wa kuhubiri fundisho hilo na kweli hizo tatu waliambatanisha na fundisho la IMANI KIYAHUDI ambayo msingi wake ni AGANO la Kale kuonyesha uvuvio na kutimizwa kwa agano la Kale. Soma mahubiri ya Petro, Stephano na Paulo ili uone namna ambavyo mtiririko ulikuwa na namna ambavyo agano la Kale limeungana na AGANO JIPYA
Matendo ya Mitume 2:14
Lakini Petro akasimama pamoja na wale kumi na mmoja, akapaza sauti yake, akawaambia, Enyi watu wa Uyahudi, na ninyi nyote mkaao Yerusalemu, lijueni jambo hili, mkasikilize maneno yangu.

Matendo ya Mitume 2:15
Sivyo mnavyodhani; watu hawa hawakulewa, kwa maana ni saa tatu ya mchana;

Matendo ya Mitume 2:16
lakini jambo hili ni lile lililonenwa kwa kinywa cha nabii Yoeli,

Matendo ya Mitume 2:17
Itakuwa siku za mwisho, asema Mungu, nitawamwagia watu wote Roho yangu, na wana wenu na binti zenu watatabiri; na vijana wenu wataona maono; na wazee wenu wataota ndoto.

Matendo ya Mitume 2:18
Naam, na siku zile nitawamwagia watumishi wangu wanaume na wanawake Roho yangu, nao watatabiri.

Matendo ya Mitume 2:19
Nami nitatoa ajabu katika mbingu juu, na ishara katika nchi chini, damu na moto, na mvuke wa moshi.

Matendo ya Mitume 2:20
Jua litageuka kuwa giza, na mwezi kuwa damu, kabla ya kuja ile siku ya Bwana iliyo kuu na iliyo dhahiri.

Matendo ya Mitume 2:21
Na itakuwa kila atakayeliitia jina la Bwana ataokolewa.

Matendo ya Mitume 2:22
Enyi waume wa Israeli, sikilizeni maneno haya: Yesu wa Nazareti, mtu aliyedhihirishwa kwenu na Mungu kwa miujiza na ajabu na ishara, ambazo Mungu alizifanya kwa mkono wake kati yenu, kama ninyi wenyewe mnavyojua;

Matendo ya Mitume 2:23
mtu huyu alipotolewa kwa shauri la Mungu lililokusudiwa, na kwa kujua kwake tangu zamani, ninyi mkamsulibisha kwa mikono ya watu wabaya, mkamwua;

Matendo ya Mitume 2:24
ambaye Mungu alimfufua, akiufungua uchungu wa mauti, kwa sababu haikuwezekana ashikwe nao.

Matendo ya Mitume 2:25
Maana Daudi ataja habari zake,
Nalimwona Bwana mbele yangu siku zote,
Kwa kuwa yuko upande wa mkono wangu wa kuume, nisitikisike.

Matendo ya Mitume 2:26
Kwa hiyo moyo wangu ukapendezewa,
ulimi wangu ukafurahi;
Tena mwili wangu nao utakaa katika matumaini.

Matendo ya Mitume 2:27
Kwa maana hutaiacha roho yangu katika kuzimu;
Wala hutamtoa Mtakatifu wako aone uharibifu.

Matendo ya Mitume 2:28
Umenijuvisha njia za uzima;
Utanijaza furaha kwa uso wako.

Matendo ya Mitume 2:29
Waume, ndugu zangu, mniwie radhi, niseme kwa ujasiri mbele yenu habari za baba yetu mkuu, Daudi, ya kuwa alifariki akazikwa, na kaburi lake liko kwetu hata leo.

Matendo ya Mitume 2:30
Basi kwa kuwa ni nabii, akijua ya kuwa Mungu amemwapia kwa kiapo, ya kwamba katika uzao wa viuno vyake atamketisha mmoja katika kiti chake cha enzi;

Matendo ya Mitume 2:31
yeye mwenyewe akitangulia kuyaona haya, alitaja habari za kufufuka kwake Kristo, ya kwamba roho yake haikuachwa kuzimu, wala mwili wake haukuona uharibifu.

Matendo ya Mitume 2:32
Yesu huyo Mungu alimfufua, na sisi sote tu mashahidi wake.

Matendo ya Mitume 2:33
Basi yeye, akiisha kupandishwa hata mkono wa kuume wa Mungu, na kupokea kwa Baba ile ahadi ya Roho Mtakatifu, amekimwaga kitu hiki mnachokiona sasa na kukisikia.

Matendo ya Mitume 2:34
Maana Daudi hakupanda mbinguni; bali yeye mwenyewe anasema,
Bwana alimwambia Bwana wangu,
Keti upande wa mkono wangu wa kuume.

Matendo ya Mitume 2:35
Hata nitakapowaweka adui zako chini ya miguu yako.

Matendo ya Mitume 2:36
Basi nyumba yote ya Israeli na wajue yakini ya kwamba Mungu amemfanya Yesu huyo mliyemsulibisha kuwa Bwana na Kristo.

(Soma pia Matendo ya mitume 5:29-32; 7:2-52)

Ndani ya fundisho la mitume kulikuwa na kweli kadha ambazo zilikuwa zikitiliwa mkazo; baadhi yake ni
1: Kristo alijitoa kufa msalabani ili kutimiza kusudi la Mungu la ukombozi.
Matendo ya Mitume 2:22
Enyi waume wa Israeli, sikilizeni maneno haya: Yesu wa Nazareti, mtu aliyedhihirishwa kwenu na Mungu kwa miujiza na ajabu na ishara, ambazo Mungu alizifanya kwa mkono wake kati yenu, kama ninyi wenyewe mnavyojua;

Matendo ya Mitume 2:23
mtu huyu alipotolewa kwa shauri la Mungu lililokusudiwa, na kwa kujua kwake tangu zamani, ninyi mkamsulibisha kwa mikono ya watu wabaya, mkamwua;

(Soma pia Matendo ya mitume 3:18-21)

2: YESU KRISTO yu hai alifufuka kutoka kwa wafu.
Matendo ya Mitume 2:24
ambaye Mungu alimfufua, akiufungua uchungu wa mauti, kwa sababu haikuwezekana ashikwe nao.

Matendo ya Mitume 2:25
Maana Daudi ataja habari zake,
Nalimwona Bwana mbele yangu siku zote,
Kwa kuwa yuko upande wa mkono wangu wa kuume, nisitikisike.

Matendo ya Mitume 2:26
Kwa hiyo moyo wangu ukapendezewa,
ulimi wangu ukafurahi;
Tena mwili wangu nao utakaa katika matumaini.

Matendo ya Mitume 2:27
Kwa maana hutaiacha roho yangu katika kuzimu;
Wala hutamtoa Mtakatifu wako aone uharibifu.

Matendo ya Mitume 2:28
Umenijuvisha njia za uzima;
Utanijaza furaha kwa uso wako.

Matendo ya Mitume 2:29
Waume, ndugu zangu, mniwie radhi, niseme kwa ujasiri mbele yenu habari za baba yetu mkuu, Daudi, ya kuwa alifariki akazikwa, na kaburi lake liko kwetu hata leo.

Matendo ya Mitume 2:30
Basi kwa kuwa ni nabii, akijua ya kuwa Mungu amemwapia kwa kiapo, ya kwamba katika uzao wa viuno vyake atamketisha mmoja katika kiti chake cha enzi;

Matendo ya Mitume 2:31
yeye mwenyewe akitangulia kuyaona haya, alitaja habari za kufufuka kwake Kristo, ya kwamba roho yake haikuachwa kuzimu, wala mwili wake haukuona uharibifu.

Matendo ya Mitume 2:32
Yesu huyo Mungu alimfufua, na sisi sote tu mashahidi wake.

3: Yesu Kristo yuko mkono wa kuume wa Mungu, mbinguni

Matendo ya Mitume 1:9
Akiisha kusema hayo, walipokuwa wakitazama, akainuliwa, wingu likampokea kutoka machoni pao.
Matendo ya Mitume 2:33
Basi yeye, akiisha kupandishwa hata mkono wa kuume wa Mungu, na kupokea kwa Baba ile ahadi ya Roho Mtakatifu, amekimwaga kitu hiki mnachokiona sasa na kukisikia.

Matendo ya Mitume 2:34
Maana Daudi hakupanda mbinguni; bali yeye mwenyewe anasema, Bwana alimwambia Bwana wangu, Keti upande wa mkono wangu wa kuume.

Matendo ya Mitume 2:35
Hata nitakapowaweka adui zako chini ya miguu yako.

4: YESU ni BWANA na ndiye KRISTO
Matendo ya Mitume 2:36
Basi nyumba yote ya Israeli na wajue yakini ya kwamba Mungu amemfanya Yesu huyo mliyemsulibisha kuwa BWANA na KRISTO.

5: Imani katika jina la Yesu Kristo, ina nguvu na huleta uponyaji, wa kimwili na kiroho
Matendo ya Mitume 3:16
Na kwa imani katika jina lake, jina lake limemtia nguvu mtu huyu mnayemwona na kumjua; na imani ile iliyo kwake yeye imempatia huyu uzima huu mkamilifu mbele yenu ninyi nyote.

Matendo ya Mitume 3:17
Basi sasa, ndugu, najua ya kuwa mliyatenda haya kwa kutokujua kwenu, kama na wakuu wenu walivyotenda.

Matendo ya Mitume 3:18
Lakini mambo yale aliyohubiri Mungu tangu zamani kwa kinywa cha manabii wake wote, ya kwamba Kristo wake atateswa, ameyatimiza hivyo.

Matendo ya Mitume 3:19
Tubuni basi, mrejee, ili dhambi zenu zifutwe, zipate kuja nyakati za kuburudishwa kwa kuwako kwake Bwana;

Matendo ya Mitume 3:20
apate kumtuma Kristo Yesu mliyewekewa tangu zamani;
Matendo ya Mitume 9:34
Petro akamwambia, Ainea, Yesu Kristo akuponya; ondoka, ujitandikie. Mara akaondoka.

Matendo ya Mitume 10:43
Huyo manabii wote humshuhudia, ya kwamba kwa jina lake kila amwaminiye atapata ondoleo la dhambi.

Tangu kipindi cha MITUME kulikuwa na upotoshaji na kupigwa vita sana dhidi ya imani na matumizi ya jina la Yesu kristo
(Soma, Matendo ya mitume 4:13-22; 5:27-29,40)

Hata sasa katika zama zetu wako wahubiri, manabii, mitume, waalimu na wachungaji ambao kwa namna moja ama nyingine wanajaribu kuonyesha kwamba jina la Yesu kristo halitoshi ndiyo maana wanaweka viambata ambavyo wanaweka kama vile chumvi, mafuta, vitambaa, picha zao, n.k, mambo hayo ni kuturudisha agano la Kale yaani torati ambapo AGANO LA KALE ni kivuli. Kwa nini kujitia kwenye kongwa tena na kutumia kitu mbadala wakati kitu halisi kipo?
Wakolosai 2:13
Na ninyi mlipokuwa mmekufa kwa sababu ya makosa yenu na kutokutahiriwa kwa mwili wenu, aliwafanya hai pamoja naye, akiisha kutusamehe makosa yote;

Wakolosai 2:14
akiisha kuifuta ile hati iliyoandikwa ya kutushitaki kwa hukumu zake, iliyokuwa na uadui kwetu; akaiondoa isiwepo tena, akaigongomea msalabani;

Wakolosai 2:15
akiisha kuzivua enzi na mamlaka, na kuzifanya kuwa mkogo kwa ujasiri, akizishangilia katika msalaba huo.

Wakolosai 2:16
Basi, mtu asiwahukumu ninyi katika vyakula au vinywaji, au kwa sababu ya sikukuu au mwandamo wa mwezi, au sabato;

Wakolosai 2:17
mambo hayo ni kivuli cha mambo yajayo; bali mwili ni wa Kristo.

6: Mamlaka ya Yesu Kristo kusamehe dhambi
Matendo ya Mitume 5:31
Mtu huyo Mungu amemtukuza kwa mkono wake wa kuume, awe Mkuu na Mwokozi, awape Waisraeli toba na msamaha wa dhambi.

7: Ujazo na utendaji wa Roho Mtakatifu
Matendo ya Mitume 8:14
Na mitume waliokuwako Yerusalemu, waliposikia ya kwamba Samaria imelikubali neno la Mungu, wakawapelekea Petro na Yohana;

Matendo ya Mitume 8:15
ambao waliposhuka, wakawaombea wampokee Roho Mtakatifu;

Matendo ya Mitume 8:16
kwa maana bado hajawashukia hata mmoja wao, ila wamebatizwa tu kwa jina lake Bwana Yesu.

Matendo ya Mitume 8:17
Ndipo wakaweka mikono yao juu yao, nao wakampokea Roho Mtakatifu.

(Soma, Matendo ya mitume 8:29; 10:44-47)
8: Ubatizo wa maji mengi
Matendo ya Mitume 8:35
Filipo akafunua kinywa chake, naye, akianza kwa andiko lilo hilo, akamhubiri habari njema za Yesu.

Matendo ya Mitume 8:36
Wakawa wakiendelea njiani, wakafika mahali penye maji; yule towashi akasema, Tazama, maji haya; ni nini kinachonizuia nisibatizwe? [

Matendo ya Mitume 8:37
Filipo akasema, Ukiamini kwa moyo wako wote, inawezekana. Akajibu, akanena, Naamini ya kwamba Yesu Kristo ndiye Mwana wa Mungu.]

Matendo ya Mitume 8:38
Akaamuru lile gari lisimame; wakatelemka wote wawili majini, Filipo na yule towashi; naye akambatiza.

Matendo ya Mitume 8:39
Kisha, walipopanda kutoka majini, Roho wa Bwana akamnyakua Filipo, yule towashi asimwone tena; basi alikwenda zake akifurahi.

Matendo ya Mitume 10:47
Ni nani awezaye kuzuia maji, hawa wasibatizwe, watu waliopokea Roho Mtakatifu vile vile kama sisi?

Matendo ya Mitume 10:48
Akaamuru wabatizwe kwa Jina lake Yesu Kristo. Ndipo wakamsihi azidi kukaa siku kadha wa kadha.

9: Tumaini la mbingu mpya na nchi mpya
2 Petro 3:13
Lakini, kama ilivyo ahadi yake, mnatazamia mbingu mpya na nchi mpya, ambayo haki yakaa ndani yake.

Hilo ndilo fundisho la mitume ambalo kanisa la leo limejengwa juu yake
Mathayo 16:16
Simoni Petro akajibu akasema, Wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai.

Mathayo 16:17
Yesu akajibu, akamwambia, Heri wewe Simoni Bar-yona; kwa kuwa mwili na damu havikukufunulia hili, bali Baba yangu aliye mbinguni.

Mathayo 16:18
Nami nakuambia, Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; wala milango ya kuzimu haitalishinda.

Mathayo 16:19
Nami nitakupa wewe funguo za ufalme wa mbinguni; na lo lote utakalolifunga duniani, litakuwa limefungwa mbinguni; na lo lote utakalolifungua duniani, litakuwa limefunguliwa mbinguni.
1 Petro 2:4
Mmwendee yeye, jiwe lililo hai, lililokataliwa na wanadamu, bali kwa Mungu ni teule, lenye heshima.

1 Petro 2:5
Ninyi nanyi, kama mawe yaliyo hai, mmejengwa mwe nyumba ya Roho, ukuhani mtakatifu, mtoe dhabihu za roho, zinazokubaliwa na Mungu, kwa njia ya Yesu Kristo.

1 Petro 2:6
Kwa kuwa imeandikwa katika maandiko
Tazama, naweka katika Sayuni jiwe kuu la pembeni, teule, lenye heshima,
Na kila amwaminiye hatatahayarika.

1 Petro 2:7
Basi, heshima hii ni kwenu ninyi mnaoamini. Bali kwao wasioamini,
Jiwe walilolikataa waashi,
Limekuwa jiwe kuu la pembeni.

1 Petro 2:8
Tena,
Jiwe la kujikwaza mguu, na mwamba wa kuangusha.
Kwa maana hujikwaza kwa neno lile, wasiliamini, nao waliwekwa kusudi wapate hayo.

1 Petro 2:9
Bali ninyi ni mzao mteule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu wa milki ya Mungu, mpate kuzitangaza fadhili zake yeye aliyewaita mtoke gizani mkaingie katika nuru yake ya ajabu;

1 Petro 2:10
ninyi mliokuwa kwanza si taifa, bali sasa ni taifa la Mungu; mliokuwa hamkupata rehema, bali sasa mmepata rehema.

Mwamba ni YESU KRISTO hivyo kanisa limejengwa juu ya Kristo

MAISHA YA MITUME 12 WA YESU KRISTO

MAISHA YA MITUME 12 WA AGANO JIPYA

Katika somo hili tutajifunza kwa kufuata vipengele vifuatavyo:-

  1. Asilia na maana ya neno Mtume
  2. Fundisho na imani ya mitume
  3. Maisha na kifo cha kila mtume
  4. Mitume katika kanisa la sasa

A:- ASILIA NA MAANA YA NENO MTUME
MTUME ni neno lililotokana na neno la kigiriki Apostolos lenye maana ya “ALIYETUMWA”. Hivyo mtume ni mtu ALIYETUMWA kupeleka ujumbe wa injili ya Yesu Kristo.
Mitume walihubiri/kueneza mafundisho ya kibiblia kuhusu imani ya dini ya kikristo na nguvu ya upendo wa Mungu kwa mwanadamu. Dhamira ya mtume ni kumhubiri Yesu Kristo, kazi yake ya ukombozi wa mwanadamu, maisha yake, kifo chake na kufufuka kwake (1 Wakorintho 15:1- 8
Basi, ndugu zangu, nawaarifu ile injili niliyowahubiri; ambayo ndiyo mliyoipokea, na katika hiyo mnasimama, na kwa hiyo mnaokolewa; ikiwa mnayashika sana maneno niliyowahubiri isipokuwa mliamini bure. Kwa maana naliwatolea ninyi hapo mwanzo yale niliyoyapokea mimi mwenyewe, ya kuwa Kristo alikufa kwa ajili ya dhambi zetu, kama yanenavyo maandiko; na ya kuwa alizikwa; na ya kuwa alifufuka siku ya tatu, kama yanenavyo maandiko;
na ya kuwa alimtokea Kefa; tena na wale Thenashara; baadaye aliwatokea ndugu zaidi ya mia tano pamoja; katika hao wengi wanaishi hata sasa, ila baadhi yao wamelala; baadaye akamtokea Yakobo; tena na mitume wote; na mwisho wa watu wote, alinitokea mimi, kama ni mtu aliyezaliwa si kwa wakati wake.)

NANI ALIANZISHA KIKUNDI HIKI?
Kikundi hiki cha mitume kilianzishwa na Yesu Kristo mwenyewe. Mitume hawa walikuwa 12 na walikuwa watu wa karibu sana na YESU KRISTO na walikuwa wanamsaidia sana katika kueneza injili
Mitume hao ni wafuatao:-
1: Simon Petro. 2: Simon Mkananayo(Zelothe
3: Yakobo mwana wa Zebedayo
4: Bartholomayo 5: Yohana mwana wa Zebedayo
6: Tomaso 7: Filipo
8: Mathayo (Lawi)
9: Yakobo mwana wa Alfayo
10: Thadayo/Yuda wa Zelote
11: Andrea 12: Yuda Iskariote
Mathayo 10:2-4, Mathayo 4:18-22, Marko 1: 16-20, 3:13-19

Mitume walikuwa na kazi ya
A.Kuhubiri ufalme wa Mungu ( Mathayo 10: 7)
B. Kuponya wagonjwa na walioonewa na shetani (Mathayo 10: 8)

Katika nyaraka zake Paulo anajitambulisha Kuwa pia MTUME wa mataifa aliyeitwa na YESU KRISTO aliyefufuka
(Matendo ya Mitume 9:15 – 16
Lakini Bwana akamwambia, Nenda tu; kwa maana huyu ni chombo kiteule kwangu, alichukue Jina langu mbele ya Mataifa, na wafalme, na wana wa Israeli. Maana nitamwonyesha yalivyo mengi yatakayompasa kuteswa kwa ajili ya Jina langu)
Paulo aliingia kwenye orodha ya mitume kutokana na kuitwa na Yesu Kristo akiwa anakwenda Dameski na kuagizwa kupeleka injili kwa mataifa kwani sifa ya Kuwa mtume ni Kuwa umewahi kumwona YESU KRISTO Paulo alimwona YESU KRISTO (1 Wakorintho 9:1- 2
Je! Mimi si huru? Mimi si mtume? Mimi sikumwona Yesu Bwana wetu? Ninyi si kazi yangu katika Bwana?
Kwa maana ikiwa mimi si mtume kwa wengine, lakini ni mtume kwenu ninyi; kwa maana ninyi ndinyi muhuri ya utume wangu katika Bwana.)

Itaendelea tena siku nyingine

MSHUKURU MUNGU KWA HURUMA ZAKE

Maombolezo 3:22-23
22 Ni huruma za Bwana kwamba hatuangamii, Kwa kuwa rehema zake hazikomi. 23 Ni mpya kila siku asubuhi; Uaminifu wako ni mkuu
MAELEZO

Ni nini kilikutegemeza usiku? Je! Utapata nini leo? Ni nini kitakachokuwezesha kufikia, hata kufanikiwa, katika siku zijazo? Huruma za BWANA. Rasilimali hizi nzuri hazijaisha kabisa! Kila siku mpya huleta ugavi mpya wao. Mungu ni mwaminifu kuhakikisha tunazo kila siku. Mungu asifiwe kwa kuifanya dunia yetu iwe mpya na iwe safi kila siku mpya
OMBI

Asante, Mungu mtakatifu na Baba mwenye upendo, kwa kunitegemeza usiku kucha na kuniahidi siku isiyo na mwisho mwishoni mwa safari yangu ya maisha. Naomba wewe, Baba yangu wa mbinguni, upate upendo na sifa kwenye midomo yangu na moyoni mwangu wakati wote. Kwa jina la Yesu. Amina.

NI WAKATI WA ZAMU YAKO

Mara nyingi tunaishi kwa vipindi na ZAMU katika dunia tuliyopo na wakati was ZAMU unapowaidia tunakuwa na majukumu ya kufanya katika kipindi hicho pasipo kujali idadi na Hali tuliyonayo

Maandiko yanasema “msiogope enyi kundi dogo kwa kuwa Baba yenu ameona vyema kuwapa ule ufalme” (Luka12:32). Hivyo kwa nanna yoyote na kwa idadi yoyote Mungu anakuwa ameturidhia kwa yeye huutazama moyo

Hatupaswi kunyamaza kwa sababu sisi no Chumvi na Nuru ya ulimwengu (mathayo5:13-16); Hivyo popote tulipo tunapaswa kusimama Katika ZAMU zetu vyema

Ikumbukwe kuwa Mungu anataka mtu mmoja tu atakae tenda kwa ya uaminifu (Yere 5:1; Malaki 1: 10)

Mfano: – Isaya 62:6-12

Mwana wa Mungu fanya kazi ya Bwana usiogope umeaminiwa